-
Kwa nini Trump anataka Pakistan iwe na uhusiano wa kawaida na utawala ghasibu wa Israel?
May 27, 2026 13:29Chanzo kimoja cha habari cha Pakistan kimeripoti kuhusu upinzani wa wazi wa Islamabad dhidi ya ombi la Rais Donald Trump wa Marekani la kuitaka nchi hiyo ijiunge na mchakato wa kuanzisha uhusiano wa kawaida na utawala haramu wa Israel, na kuongeza kuwa Islamabad inaiona hatua ya Washington kuwa jaribio la kutumia vibaya diplomasia ya "kusimamisha vita na Iran" ili kutoa mashinikizo katika kesi zisizohusiana.
-
Rais wa Iran ahimiza mshikamano wa Kiislamu dhidi ya Marekani na Israel katika mazungumzo na viongozi wa Kiislamu
May 27, 2026 10:57Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Mheshimiwa Masoud Pezeshkian, ametoa wito wa kuimarishwa umoja na ushirikiano miongoni mwa nchi za Kiislamu, akisisitiza kuwa mshikamano wa Umma mzima wa Kiislamu ni nguzo muhimu katika kukabiliana na vitisho na changamoto zinazokabili eneo la Magharibi mwa Asia.
-
Iran yasema ukiukwaji wa makubaliano ya kusitisha vita unathibitisha “nia ovu” ya Marekani,
May 27, 2026 10:53Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imelaani vikali ukiukwaji wa “wazi na usio na msingi” wa makubaliano ya kusitisha mapigano uliofanywa na Marekani katika Lango Bahari la Hormuz.
-
Hizbullah yatekeleza operesheni 32 dhidi ya majeshi ghasibu ya Israel kusini mwa Lebanon
May 27, 2026 10:51Harakati ya Mapambano ya Kiislamu nchini Lebanon, Hizbullah, imetangaza kutekeleza mfululizo wa operesheni 32 za kijeshi dhidi ya majeshi vamizi ya utawala wa Kizayuni wa Israel yanayofanya chokochoko kusini mwa nchi hiyo.
-
Wapalestina wa Gaza katika jinamizi badala ya sherehe wakati wa Eid el-Adha
May 27, 2026 10:43Ikiwa leo ni sikukuu ya Eid El-Adha, Wapalestina wanaoishi katika Ukanda wa Gaza eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na utawala wa Kizayuni wa Israel hawana cha kusherehekea bali wanakumbwa na jinamizi na masaibu yaliyosababishwa na utawala huo ghasibu.
-
Serikali ya DRC yasitisha safari za ndege Bunia kufuatia mlipuko wa Ebola
May 27, 2026 10:40Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) imechukua hatua ya dharura kwa kusitisha safari zote za ndege zinazoingia na kutoka mjini Bunia, mashariki mwa nchi hiyo, ikiwa ni juhudi za kudhibiti kuenea kwa ugonjwa hatari wa Ebola.
-
IRGC yaitungua ndege ya kivita ya Marekani katika Ghuba ya Uajemi, yatoa onyo kali
May 27, 2026 03:24Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetangaza kuwa vitengo vyake vya ulinzi wa anga vimetungua ndege ya kivita ya Marekani isiyo na rubani, aina ya MQ-9 Reaper, katika anga ya Ghuba ya Uajemi.
-
Iran yaonya kuwa, ikishambuliwa tena jibu la litakuwa ‘kali zaidi’ kuliko vita vilivyopita
May 27, 2026 03:16Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran limetoa onyo kali kuhusu mashambulizi ya kulipiza kisasi yatakayokuwa “mazito na makali zaidi” iwapo tawala za Marekani na Israel zitafanya uchokozi mpya.
-
Pakistan yakataa wito wa Marekani wa kuanzisha uhusiano na 'Israel'
May 27, 2026 03:12Pakistan imekataa wito wa Rais wa Marekani, Donald Trump, wa kuitaka kuanzisha uhusiano wa kawaida na utawala haramu wa Israel. Waziri wa Ulinzi wa Pakistan, Khawaja Asif, amesema pendekezo hilo kuwa “halikubaliki” na linakwenda kinyume na misingi ya taifa hilo.
-
Russia yaunga mkono msukumo wa Afrika wa kudai fidia kutoka kwa madola ya kikoloni
May 27, 2026 03:06Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia, Sergey Lavrov, amesema nchi yake inaunga mkono msukumo wa Afrika wa kutaka fidia kutoka kwa madola ya kikoloni. Akizungumza katika hafla ya kuadhimisha Siku ya Afrika mjini Moscow, Lavrov amesema suala hilo ni sehemu ya mapambano mapana dhidi ya ukoloni mambo-leo.