-
Mamilioni ya Wairani wamuomboleza Kiongozi Muadhamu; taifa lazizima
Mar 01, 2026 02:44Wananchi wa Iran wamemiminika mitaani na katika medani mbali mbali kumuomboleza Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, aliyeuawa shahidi katika shambulizi la kigaidi la Marekani na utawala haramu wa Israel.
-
Larijani: Taifa la Iran litawafanya maadui wajutie uchokozi wao
Mar 01, 2026 02:20Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran, Ali Larijani amesema taifa hili litazifanya Marekani na Israel kujutia uchokozi wao dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu.
-
Katibu Mkuu wa UN: 'Uhamiaji si mgogoro', ahimiza ushirikiano wa kimataifa
Feb 28, 2026 02:33Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, amezitolea wito nchi mbalimbali kupinga simulizi zinazochochewa na hofu kuhusu suala la uhamiaji, akisisitiza kwamba "uhamiaji si mgogoro".
-
Amnesty International: Upanuzi wa Israel wa vitongoji vya walowezi katika Ukingo wa Magharibi ni changamoto dhahiri kwa sheria za kimataifa
Feb 28, 2026 02:32Shirika la Amnesty International limetangaza kwamba tangu mwezi Disemba mwaka jana, serikali ya Israel imezidisha harakati zake katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu huko Palestina, ikiwa ni pamoja na Quds Mashariki (Yerusalemu Mashariki), kupitia mfululizo wa maamuzi ambayo imesema yanalenga kuimarisha unyakuzi wa ardhi hiyo.
-
Guinea imewaachia huru wanajeshi 16 wa Sierra Leone waliokamatwa mapema wiki hii
Feb 28, 2026 02:32Katika hatua inayolenga kupunguza mvutano, Sierra Leone imesema kuwa Guinea jana iliwaachilia huru wanajeshi na maafisa wake wa polisi 16 waliokamatwa siku ya Jumanne.
-
Polisi Kenya kukabiliana na ongezeko la ukosefu wa amani mijini kipindi cha Uchaguzi Mkuu
Feb 28, 2026 02:30Idara ya Polisi ya Kenya imetangaza mipango ya kuunda vikosi maalumu cha kukabiliana na ongezeko la ukosefu wa usalama jijini Nairobi na katika miji mingine mikubwa huku nchi ikielekea katika kipindi cha kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2027.
-
Wimbi jipya la upinzani dhidi ya vita nchini Marekani; dalili ya kudhoofika zaidi Trump
Feb 28, 2026 02:11Kadiri matamshi ya kivita yanavyozidi kutoka kwa Rais wa Marekani, Donald Trump, pamoja na baadhi ya maafisa wa utawala wake, wimbi jipya la upinzani dhidi ya uwezekano wa a vita vya kichochezi vya Marekani dhidi ya Iran limeanza kushika kasi.
-
Iran yahimiza kusitishwa mapigano mara moja kati ya Afghanistan na Pakistan
Feb 28, 2026 02:00Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imezitaka Pakistan na Afghanistan kuketi kwenye meza ya mazungumzo haraka iwezekanavyo ili kusimamisha mapigano na kupunguza mvutano, huku mapigano ya mpakani kati ya nchi hizo mbili yakizidi kupamba moto.
-
Iran: Mafanikio ya mazungumzo ya nyuklia yanategemea kuwa jadi Marekani
Feb 27, 2026 22:59Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi amesisitiza kwamba, mazungumzo ya nyuklia yasiyo ya moja kwa moja kati ya Jamhuri ya Kiislamu na Marekani yatafanikiwa tu iwapo Washington itayachukuliwa kwa uzito na kuzingatia uhalisia wa mambo.
-
OIC yaonya dhidi ya vitisho vya kuishambulia kijeshi Iran
Feb 27, 2026 22:55Kamati ya Utendaji ya Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) imeonyesha wasiwasi wake kuhusu vitisho vya hivi karibuni dhidi ya Iran.