-
Iran: Kutochukua hatua Baraza la Usalama dhidi ya jinai za Israel ni 'janga'
Feb 27, 2026 22:52Iran imelishutumu Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa kufumbia macho mashambulizi mabaya yaliyofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Lebanon, ambayo yanakiuka makubaliano ya kusitisha mapigano ya 2024.
-
Israel yaendelea kuwazuia Wapalestina kuswali Masjidul Aqsa
Feb 27, 2026 22:49Jeshi la Israel jana lilipeleka idadi kubwa ya wanajeshi katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu, hasa katika vituo vya ukaguzi vinavyoelekea katika mji wa Quds (Jerusalem), sanjari na kuimarisha vizuizi dhidi ya Wapalestina waliotaka kuingia katika Msikiti wa al-Aqsa kwa ajili ya Swala ya Ijumaa ya pili ya mwezi mtukufu wa Ramadhani.
-
UNHCR: Sudan Kusini ina wakimbizi zaidi ya 600,000
Feb 27, 2026 22:47Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR) limesema Sudan Kusini ni mwenyeji wa wakimbizi na waomba hifadhi 613,710 katika kaya 164,574 katika majimbo 29 kote nchini.
-
Katika mwaka 2025, wahamiaji wapatao elfu nane wamefariki au kutoweka duniani kote
Feb 27, 2026 05:41Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji (IOM) limetangaza kuwa watu wasiopungua 7,667 walifariki au kutoweka katika njia za uhamiaji duniani kote katika mwaka uliopita wa 2025, na kuonya kwamba idadi halisi ya watu hao huenda ikawa kubwa zaidi huku likiitaja hasara hiyo ya upoteaji wa roho za watu inayoendelea kushuhudiwa kuwa "kufeli kimataifa."
-
Sera ya kikanda ya Iran: Imejikita katika kudumisha amani, utulivu na kutotegemea madola nje ya eneo
Feb 27, 2026 03:45Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza katika mazungumzo na Waziri wa Ulinzi wa Armenia kuhusu azma ya Iran ya kustawisha na kuimarisha uhusiano wa pande mbilii na majirani zake hasa Armenia.
-
Pakistan yatangaza 'vita vya wazi' dhidi ya Afghanistan, yashambulia Kabul na miji mingine
Feb 27, 2026 03:43Waziri wa Ulinzi wa Pakistan amesema, subira ya nchi yake kwa kundi la Taliban imemalizika na kwa hiyo imeingia kwenye "vita vya wazi," dhidi ya Afghanistan.
-
UN: Wakimbizi wa Burundi walioko Tanzania wanarudi makwao kwa hiari, hawashurutishwi
Feb 27, 2026 03:27Afisa wa Uhusiano wa Nje wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR nchini Tanzania Bahia Egeh amesema, wakimbizi wa Burundi walioko nchini humo ambao wanarudi makwao, wanafanya hivyo kwa hiari wala hawashurutishwi.
-
Araghchi: Iran na US zinapiga hatua 'karibu zaidi kufikia mwafaka' katika baadhi ya masuala
Feb 27, 2026 00:01Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Sayyid Abbas Araghchi amesema duru ya karibuni ya mazungumzo yasiyo ya ana kwa ana na Marekani iliyofanyika jana mjini Geneva, Uswisi ilikuwa moja ya mazungumzo bora, mazito zaidi, na marefu zaidi kuwahi kufanyika hadi sasa, na kwamba Tehran na Washington zimepiga hatua za "karibu zaidi kufikia mwafaka" katika baadhi ya masuala.
-
El-Baradei, mkuu wa zamani wa IAEA aionya Marekani kuhusu gharama “za kutisha” za vita dhidi ya Iran
Feb 26, 2026 23:19Mohamed El-Baradei, aliyewahi kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki (IAEA), ameionya Marekani kuhusu madhara makubwa na ya kutisha yatakayojitokeza iwapo itaingia katika vita vingine dhidi ya Iran, huku akipinga hoja za Washington zinazodai kuhalalisha uchokozi huo mpya.
-
Baraza la Usalama la UN lawaadhibu makamanda wa RSF kwa ukatili wa Darfur
Feb 26, 2026 23:19Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limewawekea vikwazo makamanda wanne wa kundi la waasi la Rapid Support Forces (RSF) linalopigana na jeshi la Sudan, wanaoshukiwa kufanya ukatili dhidi ya raia ambao wataalamu wa Umoja wa Mataifa wanasema ulikuwa na "ishara za mauaji ya kimbari."