-
Wademokrati wanaishutumu Wizara ya Sheria ya Marekani kwa kumwondoa Trump kwenye Mafaili ya Epstein
Feb 26, 2026 23:08Chama cha Democratic kimeituhumu serikali ya Rais wa Marekani, Donald Trump, kwa "ufichaji mkubwa zaidi wa serikali katika historia ya sasa" kutokana na ripoti kwamba imeficha nyaraka zinazohusiana na madai kwamba rais Trump anayetoka chama cha Republican alimnyanyasa kingono mtoto mdogo.
-
Kim atishia kuifuta kabisa Korea Kusini na kuweka masharti ya makubaliano na Washington
Feb 26, 2026 23:08Kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong Un, ametishia "kumfuta kabisa" jirani yake wa kusini iwapo usalama wa nchi yake utatishiwa, akiitaja Korea Kusini kuwa ndiyo "kitu chenye uadui mkubwa zaidi" na kutupilia mbali uwezekano wowote wa kufanya mazungumzo na nchi hiyo.
-
Senegal inapendekeza sheria kali zaidi dhidi ya vitendo vya mahusiano ya jinsia moja
Feb 26, 2026 07:26Waziri Mkuu wa Senegal amependekeza sheria mpya itakayoongeza adhabu dhidi ya mahusiano ya jinsia moja, ambapo watakaopatikana na hatia wanaweza kuhukumiwa kifungo cha hadi miaka kumi jela.
-
Araghchi: Marekani inapaswa kuacha misimamo ya kukinzana
Feb 26, 2026 02:53Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Sayyid Abbas Araghchi amesema kwamba mafanikio ya mazungumzo yatategemea upande wa pili kuyachukuliwa kwa uzito na kujiepusha na tabia na misimamo inayokinzana.
-
Iran yapinga “uongo mkubwa” wa Marekani kuhusu kadhia ya nyuklia
Feb 26, 2026 02:43Iran imepinga vikali madai mapya ya Marekani kuhusu shughuli zake za nyuklia na makombora, pamoja na takwimu za waliouawa katika machafuko ya hivi karibuni, ikiyataja kuwa ni “msururu wa uongo mkubwa” huku ikikosoa kampeni iliyoratibiwa ya upotoshaji wa taarifa dhidi yake.
-
Upeo wa ubaguzi; Trump ataka Ilhan, Tlaib wafukuzwe Marekani
Feb 26, 2026 02:06Rais Donald Trump amesema Wawakilishi wa Marekani, Ilhan Omar na Rashida Tlaib wanapaswa kurudishwa "walikotoka" baada ya wabunge hao wawili wa chama cha Democratic katika Congress ya Marekani kupiga kelele na kulalamika wakati wa hotuba ya karibuni ya Trump katika Kongresi.
-
CPJ: Israel ndiyo iliyoua wanahabari wengine zaidi duniani 2025
Feb 26, 2026 01:54Utawala haramu wa Israel uliwaua wanahabari wasiopungua 84 mwaka wa 2025 - idadi kubwa zaidi kuliko dola lolote duniani katika mwaka uliokuwa mbaya zaidi kuwahi kurekodiwa kwa vyombo vya habari.
-
Makumi wauawa katika mashambulizi pacha ya magaidi Nigeria
Feb 26, 2026 01:40Watu wasiopungua 25 wameuawa huku nyumba kadhaa zikichomwa moto baada ya watu wenye silaha kushambulia vijiji viwili katika Jimbo la Adamawa, kaskazini mashariki mwa Nigeria usiku wa kuamkia jana.
-
Waafrika 1,700 wadaiwa kushiriki katika vita vya Russia, Ukraine
Feb 26, 2026 01:24Waziri wa Mambo ya Nje wa Ukraine, Andrii Sybiha amedai kwamba, zaidi ya Waafrika 1,700 wanapigana kwa niaba ya Russia katika vita vyake dhidi ya Ukraine, na kuongeza kwamba Moscow inatumia hadaa kuwasajili jeshini raia hao wa Kiafrika.
-
Iran yamuonya Trump asichukue maamuzi yanayotegemea taarifa za uongo
Feb 26, 2026 00:21Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amemuonya Rais wa Marekani Donald Trump dhidi ya kufanya maamuzi yanayotegemea taarifa zisizo sahihi, akisisitiza kuwa Iran haijawahi kutafuta, haitafuti, wala haitawahi kutafuta silaha za nyuklia.