-
Ghannouchi, akiwa gerezani: Mustakabali wa Tunisia ni uhuru, "hata kama itachukua muda"
Feb 23, 2026 03:38Mkuu wa harakati ya Kiislamu ya Ennahda, Rached Ghannouchi, amesema kwamba mustakabali wa Tunisia ni uhuru, utawala wa sheria na kubadilishana madaraka kwa amani "hata kama itachukua muda."
-
Waislamu wa kaunti kame Kenya walalamikia ukosefu wa maji katika mwezi Ramadhani
Feb 23, 2026 03:36Viongozi wa kidini nchini Kenya wamelalamika kuhusu hali ya ukame inayokumba kaunti zenye idadi kubwa ya Waislamu huku waumini wakiwa katika mfungo wa Ramadhani.
-
Kamanda wa Iran apuuzilia mbali hatua ya US ya kutuma meli za kivita Asia Magharibi; asema ni ya kimaonyesho
Feb 23, 2026 00:10Kamanda wa jeshi la Iran amepuuzilia mbali mkusanyiko wa meli na ndege za kivita za Marekani katika eneo la Asia Magharibi zilizoshuhudiwa wiki chache za hivi karibuni na kuitaja kuwa hatua ya kimaonyesho" huku kukiwa na mvutano kuhusu mpango wa nyuklia wa Tehran na kwamba Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu ametoa jibu madhubuti kwa hila hizo za hali ya juu.
-
Marekani yashangaa kwa nini Iran haijasalimu amri licha ya mashinikizo ya kijeshi
Feb 23, 2026 00:10Mjumbe maalum wa Marekani katika eneo la Asia Magharibi, Steve Witkoff, amesema kuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameonyesha mshangao mkubwa kuhusu sababu zinazofanya Iran isikubali masharti ya Washington katika mazungumzo yanayohusu mpango wake wa nyuklia.
-
Ansarullah yalaani mauaji ya umati ya umwagaji damu ya Israel mashariki mwa Lebanon
Feb 23, 2026 00:09Harakati ya Ansarullah ya Yemen imelaani vikali "mauaji ya umati ya umwagaji damu" yaliyofanywa na utawala wa Israel katika eneo la Beqaa mashariki mwa Lebanon, na kuuwa takriban watu kumi na kujeruhi wengine wengi.
-
Machungu ya ukoloni: Pamba, moto, na njaa; faili la umwagaji damu la Ujerumani Afrika Mashariki
Feb 23, 2026 00:08Ukoloni katika karne ya 19 na 20 haukuwa tu ukihusiana na kueneza bendera katika ramani ya dunia; bali ulikuwa mradi uliopangwa wa kutwaa ardhi, rasilimali, na nguvukazi ambao ulibadilisha miundo ya kiuchumi na kijamii ya watu waliokuwa chini ya ukoloni.
-
Kiongozi wa Ansarullah: Marekani ni mshirika wa adui Mzayuni katika jinai zake zote
Feb 23, 2026 00:08Kiongozi wa Harakati ya Ansarullah ya Yemen, ameashiria kile kinachojulikana kama "Bodi ya Amani ya Trump" kwa ajili ya Gaza, na kusema: "Marekani ni mshirika wa adui Mzayuni katika jinai zake zote."
-
Wamarekani wahoji: Je, Huckabee anawakilisha maslahi ya Washington au Tel Aviv?
Feb 22, 2026 23:44Kauli na matamshi ya balozi wa Marekani huko Israel, Mike Huckabee, yamesababisha hasira kubwa baada ya kusema kwamba utawala ghasibu wa Israel una haki ya kupanua eneo lake kwa kupora eneo kubwa la Mashariki ya Kati la nchi kadhaa za Kiarabu na Kiislamu, kwa mujibu wa tafsiri maarufu za Torati ndani ya harakati za Kikristo yenye msimamo mkali nchini Marekani.
-
Sudan: Kumpokea Hemedti huko Uganda ni "uungaji mkono wa moja kwa moja kwa mauaji ya kimbari"
Feb 22, 2026 10:19Wizara ya Mambo ya Nje ya Sudan imelaani vikali hatua ya serikali ya Uganda ya kumpokea kamanda wa waasi wa Rapid Support Forces (RSF), Mohamed Hamdan Dagalo (Hemedti), ikielezea hatua hiyo kuwa ni "msaada wa moja kwa moja kwa uhalifu wa mauaji ya kimbari."
-
Waziri Araghchi: Iran italinda haki za taifa katika nyuklia kupitia diplomasia
Feb 22, 2026 08:54Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amesisitiza dhamira ya nchi yake kulinda haki halali za taifa katika nyanja ya nishati ya nyuklia kwa njia ya diplomasia.