-
China, Russia zasisitiza kutatuliwa kidiplomasia kadhia ya nyuklia ya Iran
Feb 21, 2026 22:46Wawakilishi wa Russia na China katika mashirika ya kimataifa yenye makao yake mjini Vienna Austria wamesisitiza suluhisho la kidiplomasia kwa suala la nyuklia la Iran.
-
WFP kusimamisha huduma ya msaada wa chakula nchini Somalia
Feb 21, 2026 22:46Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limetangaza kuwa, huenda likasitisha msaada na harakati zake za kibinadamu nchini Somalia ifikapo mwezi Aprili mwaka huu sababu ni ufadhili mpya kutopatikana haraka.
-
WHO: Makumi ya watu wameuawa katika mashambulio dhidi ya vituo vya afya Sudan
Feb 21, 2026 22:45Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza kuwa, makumi ya watu wameuawa kufuatia mashambulio dhidi ya vituo vya afya nchini Sudan.
-
Afisa wa EU awashinikiza waasi wa DR Congo kufungua njia za kibinadamu
Feb 21, 2026 22:45Kamishna wa Umoja wa Ulaya, anayehusika na masuala ya misaada ya kibinadamu, amewasihi waasi wa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kufungua njia za kibinadamu kwa ajili ya kupata misaada mamilioni ya raia mashariki mwa nchi hiyo inayokabaliwa na machafuko.
-
Shirikisho la Soka Senegal lapinga hukumu ya mashabiki wao Morocco
Feb 21, 2026 22:44Shirikisho la Soka la Senegal (FSF) limelaani hukumu iliyotolewa na Mahakama ya Morocco dhidi ya mashabiki 18 wa Senegal waliopatikana na hatia ya kufanya vurugu kufuatia fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika, AFCON.
-
Ansarullah: Kujizatiti upya kijeshi maadui katika eneo ni ishara kwamba Muqawama ungali hai
Feb 21, 2026 07:38Mjumbe mwandamizi wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Yemen ya Ansarullah ametoa taarifa akieleza kwamba kuzungumziwa duru mpya ya vita vinavyotaka kuanzishwa dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Muqawama ni sawa na adui kukiri kwamba alishindwa katika vita vilivyopita.
-
Licha ya vizuizi vikali vya Israel, Wapalestina laki moja wasali I'sha na Tarawehe Masjidul-Aqsa
Feb 21, 2026 07:37Licha ya vizuizi vikali vilivyowekwa na utawala wa Kizayuni wa Israel vya kuingia katika Msikiti wa Al-Aqsa, makumi ya maelfu ya Wapalestina jana usiku walihudhuria katika msikiti huo mtukufu kusali Sala za I'sha na Tarawehe wakati huu wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.
-
Kenya yaitaka Russia iirejeshee miili na raia wake waliofungwa katika vita vya Ukraine
Feb 21, 2026 07:37Serikali ya Kenya imeitaka Russia iirejeshe nyumbani miili ya raia wake waliouawa na wale waliokamatwa kama wafungwa wa vita, ambao wameripotiwa kuwa walipiigania Russia katika vita na Ukraine.
-
Watu 50 wauawa katika shambulio la wabeba silaha kaskazini magharibi ya Nigeria
Feb 21, 2026 07:36Kundi moja la wabeba silaha limewaua watu wasiopungua 50 na kuwateka nyara wanawake na watoto katika shambulio la usiku kwenye kijiji kimoja kilichoko kaskazini magharibi mwa Jimbo la Zamfara nchini Nigeria.
-
Uhispania: Ilikuwa ni 'makosa' Kamishna wa EU kuhudhuria mkutano wa 'Bodi ya Amani' ya Trump
Feb 21, 2026 07:35Waziri wa Mambo ya Nje wa Uhispania Jose Manuel Albares amesema, ilikuwa ni "makosa" kwa Kamishna wa Umoja wa Ulaya kuhudhuria mkutano wa uzinduzi wa 'Bodi ya Amani' ya Rais wa Marekani Donald Trump mjini Washington.