-
Mtazamo wa Moscow kuhusu maneva ya pamoja ya baharini kati ya Iran, Russia na China
Feb 21, 2026 05:41Moscow imetangaza kuwa mazoezi ya pamoja ya majini kati ya majeshi ya Iran, Russia na China yatafanyika katika Lango -Bahari la Hormuz.
-
Iran yaonya kuhusu wapenda vita wanaotaka “vita vya maafa”
Feb 21, 2026 04:09Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa Marekani haijawahi kudai kusitishwa kabisa kwa urutubishaji wa urani katika mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja yanayoendelea, huku akionya kuwa baadhi ya wenye misimamo mikali wanajaribu kuisukuma sera ya Marekani kuelekea katika “vita visivyo vya lazima na vya maafa.”
-
Guinea-Bissau yasitisha utafiti wa chanjo unaofadhiliwa na Marekani
Feb 21, 2026 04:07Guinea-Bissau imesitisha utafiti tata wa chanjo ya homa ya ini aina ya B (Hepatitis B) uliokuwa ukifadhiliwa na utawala wa Rais wa Marekani Donald Trump, baada ya Shirika la Afya Duniani (WHO) kueleza wasiwasi mkubwa wa kimaadili kuhusu muundo wa utafiti huo.
-
WFP: Somalia inakabiliwa na hatari ya baa la njaa
Feb 21, 2026 04:06Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani WFP limesema hali ya upatikanaji wa chakula nchini Somalia imefikia hatua mbaya ambapo mamilioni ya watu wako hatarini kukumbwa na njaa kali kutokana na ukosefu wa fedha za msaada.
-
Balozi wa Marekani: Ni sawa ikiwa Israel itanyakua ardhi kote Asia Magharibi
Feb 21, 2026 04:05Balozi wa Marekani katika utawala Israel amesema itakuwa “sawa tu” iwapo utawala wa Kizayuni wa Israel utapanua mipaka yake kote katika Asia Magharibi chini ya mpango wa “Israeli Kubwa.”
-
Wabunge wa Marekani wanataka kupiga kura kuzuia mamlaka ya Trump ya kushambulia Iran
Feb 21, 2026 04:05Wabunge wa Marekani huenda wakapiga kura mapema wiki ijayo juu ya muswada unaolenga kumzuia Rais Donald Trump kuanzisha mashambulizi ya kijeshi dhidi ya Iran bila idhini ya wazi ya Bunge la Marekani.
-
Mwandishi wa NY Times: Netanyahu anamtumia vibaya Trump kwa ajili ya vita na Iran
Feb 20, 2026 23:35Mwandishi maarufu wa gazeti la Marekani la New York Times, Thomas Friedman, ameonya kwamba waziri mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu anamhadaa Rais wa Marekani, Donald Trump, na makundi ya jamii ya Wayahudi wa Marekani ili kuendeleza malengo yake ya kisiasa yenye utata, ikiwa ni pamoja na kuongezeka mvutano na Iran.
-
Ripota wa UN kuhusu Palestina asema, licha ya kuandamwa hatasalimu amri, hatajiuzulu
Feb 20, 2026 23:06Francesca Albanese, ripota maalumu wa Umoja wa Mataifa wa maeneo ya Palestina yanayokaliwa kwa mabavu, amesema hatajiuzulu wadhifa wake huo licha ya mashinikizo yanayotolewa dhidi yake na serikali za nchi kadhaa za Ulaya kutokana na matamshi yanayodaiwa kuwa ametoa dhidi ya utawala wa kizayuni wa Israel.
-
Al-Burhan: Hakutakuwa na suluhu Sudan mpaka RSF iondoke kwenye maeneo yote inayoyakalia
Feb 20, 2026 22:53Mkuu wa Baraza la Utawala la Sudan, Abdel Fattah al-Burhan, amesema hakutakuwa na usitishaji mapigano mpaka pale Vikosi vya Usaidizi wa Haraka (RSF) vitakapojiondoa kwenye kile alichokieleza kuwa ni maeneo vinayoyakalia na kujikusanya upya katika maeneo yaliyotengwa.
-
Mashabiki 18 wa Senegal wahukumiwa vifungo jela Morocco kwa yaliyojiri kwenye fainali ya AFCON
Feb 20, 2026 22:52Mahakama ya Morocco imewahukumu mashabiki 19 wa soka kifungo cha mwaka mmoja jela kwa vitendo vya kihuni walivyovionesha wakati wa mchezo wa fainali ya AFCON 2025 kati ya Morocco na Senegal, ambapo walijaribu kuvamia uwanja.