-
Kenya kufungua tena mpaka wake na Somalia baada ya kufungwa kwa miaka 15
Feb 13, 2026 07:18Rais wa Kenya William Ruto ametangaza kuwa Kenya itafungua tena mpaka wake na Somalia mwezi Aprili, baada ya kufungwa kwa muda wa miaka 15 kufuatia mashambulizi ya mara kwa mara ya kigaidi. Hatua hiyo inaashiria jaribio jipya la kurejesha harakati za mpakani na kuimarisha ushirikiano wa kikanda.
-
Maelfu waandamana Melbourne kulaani ziara ya rais wa 'Israel' nchini Australia
Feb 13, 2026 07:06Maelfu ya waandamanaji wanaounga mkono Palestina walipaza sauti na kufunga barabara kadhaa mjini Melbourne, chini ya ulinzi mkali wa mamia ya polisi, wakati Rais wa utawala haramu wa Israel Isaac Herzog akihitimisha ziara yake iliyokumbwa na utata mkubwa nchini Australia.
-
Iran yatuma satelaiti ya “Jam‑e Jam 1” angani, hatua muhimu kwa utangazaji wa kitaifa
Feb 13, 2026 07:05Shirika la Utangazaji la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran (IRIB) limetuma kwa mafanikio satelaiti yake ya kwanza maalumu kwa utangazaji, iitwayo “Jam‑e Jam 1”, inayojulikana kimataifa kama “Iran DBS”. Hatua hiyo inaashiria ngazi mpya ya kimkakati katika kuimarisha miundombinu ya vyombo vya habari vya Iran kupitia anga za juu.
-
Umoja wa Afrika wapongeza mapatano ya kusitisha vita kati ya Serikali ya DRC na waasi wa M23
Feb 13, 2026 07:02Tume ya Umoja wa Afrika (AU) imekaribisha kutiwa saini kwa kanuni za marejeo ya mfumo wa kusitisha mapigano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na muungano wa waasi wa AFC/M23.
-
Kiongozi Muadhamu awashukuru wananchi kwa kuwakatisha tamaa maadui katika maandamano ya mamilioni ya watu
Feb 13, 2026 03:51Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amewasifu na kuwapongeza wananchi wa Iran kwa kujitokeza kwa wingi kote nchini katika maandamano ya maadhimisho ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu na kusema kuwa maandamano hayo yamewakatisha tamaa maadui.
-
Palestina inavyotokomezwa kupitia ukoloni; Iran yalaani uamuzi wa Israel wa kunyakua Ukingo wa Magharibi
Feb 13, 2026 03:51Iran imelaani vikali uamuzi wa hivi karibuni wa utawala wa Israel wa kunyakua ardhi zaidi za Wapalestina katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu, ikisema kuwa hatua hiyo inalenga kupanua "ujenzi haramu wa vitongoji vya walowezi za Kizayuni" na kuimarisha ukaliaji mabavu na hatua kali za kiusalama dhidi ya Wapalestina na kuendelea "mauaji ya kimbari" huko Gaza.
-
Takriban watu 21 wameaga dunia baada ya boti kuzama katika Mto Nile, Sudan
Feb 13, 2026 03:50Takriban watu 21 wamekufa maji wakati boti iliyokuwa ikiwasafirisha ilipozama katika Mto Nile kaskazini mwa Sudan.
-
Mashambulizi ya droni ya wanamgambo wa RSF yaua watu 2 na kujeruhi 4 Kordofan, Sudan
Feb 13, 2026 03:50Mashambulizi ya ndege zisizo na rubani (droni) za wanamgambo wa kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) yameuwa raia wawili na kujeruhi wanne katika jimbo la Kordofan Kusini. Haya yamebainishwa jana Mtandao wa Madaktari wa Sudan.
-
Afrika Kusini: Ramaphosa atangaza kutumwa jeshi kukabiliana na jinai
Feb 13, 2026 03:49Katika jitihada za kupunguza viwango vya juu vya magenge ya uhalifu na jinai nyingine, Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini ametangaza kuwa atatuma jeshi ili kushirikiana na polisi katika suala hilo.
-
AU yasisitiza kuunga mkono umoja wa Somalia; yalaani kuingiliwa masuala ya ndani ya Sudan
Feb 12, 2026 23:19Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika (AU) kwa mara nyingine tena jana Alhamisi lilithibitisha kuhusu mamlaka ya kujitawala na umoja wa ardhi nzima ya Somalia na kutupilia mbali suala la kutambuliwa rasmi eneo la Somaliland kama nchi huru.