-
Mkuu wa IAEA: Iran-mwanachama wa NPT, ina haki ya kurutubisha urani
Feb 12, 2026 22:34Rafael Grossi, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki (IAEA), amesema katika mahojiano na gazeti la Financial Times kwamba, Iran kama nchi iliyotia saini Mkataba wa Kuzuia Uenezaji wa Silaha za Nyuklia (NPT), ina haki ya kurutubisha urani.
-
Kremlin: Russia haina mpango wa kushiriki mkutano wa 'Bodi ya Amani'
Feb 12, 2026 22:33Ikulu ya Russia ya Kremlin imethibitisha kwamba maafisa wa nchi hiyo hawana mpango wa kuhudhuria mkutano wa kwanza wa Bodi ya Amani (ya Gaza) uliopangwa kufanyika Februari 19 huko Washington.
-
Sudan yataka irejeshewe uanachama katika Umoja wa Afrika
Feb 12, 2026 22:32Waziri wa Mambo ya Nje wa Sudan, Muhi al-Din Salem Ahmed amekariri wito wake kwa Umoja wa Afrika, akiitaka AU kufuta hatua yake ya kuisimamishia uanachama nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika katika umoja huo.
-
Zaidi ya raia 2,000 wa UK wamepigana kwa niaba ya Israel katika mauaji ya halaiki Gaza
Feb 12, 2026 22:32Maelfu ya raia wa Uingereza wamehudumu katika jeshi la Israel wakati wa vita vya mauaji ya halaiki vya utawala huo wa Kizayuni dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza.
-
Nguvu ya majini ya Iran; mseto wa nguvu za kijeshi, diplomasia, teknolojia na maadili ya kibinadamu
Feb 12, 2026 22:30Kamanda wa Jeshi la Wanamaji la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa, uwepo wa meli za Iran katika bahari na maji ya kimataifa ni mseto wa nguvu za kijeshi na diplomasia ya baharini.
-
Pezeshkian apongeza hamasa kubwa ya wananchi waliojitokeza katika maadhimisho ya tarehe 22 Bahman
Feb 12, 2026 07:54Rais Masoud Pezeshkian amewapongeza na kuwashukuru wananchi wa Iran kwa kujitokeza kwa wingi "katika hamasa ya aina yake" katika maandamano ya kitaifa kote nchini ya maadhimisho ya kumbukumbu ya miaka 47 ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu.
-
Araqchi: Wairani waliandamana tarehe 22 Bahman kutangaza kuwa haki na utu wao haviuzwi
Feb 12, 2026 07:53Abbas Araqchi Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa umati mkubwa wa wananchi wa walioshiriki katika maandamano ya kitaifa ya kuadhimisha kumbukumbu ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya mwaka 1979 wametangaza wazi kwamba haki na utu wao haviuzwi.
-
Hamas yazionya US, Israel: Vita yoyote dhidi ya Iran ni sawa na kushambulia Ulimwengu mzima wa Kiislamu
Feb 12, 2026 07:53Brigedi za al Qassam, tawi ila kijeshi la Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imeonya kuwa vita yoyote dhidi ya Iran ni sawa na shambulio dhidi ya Umma mzima wa Kiislamu.
-
Wazimbabwe watofautiana baada ya mawaziri kupitisha mswada wa kuongeza muda wa rais kusalia madarakani
Feb 12, 2026 07:52Wazimbabwe wametofautiana kuhusu hatua ya baraza la mawaziri ya kuunga mkono muswada unaokusudia kubadilisha katiba ili kumruhusu Rais Emmerson Mnangagwa mwenye umri wa miaka 83 kubakia madarakani hadi angalau mwaka 2030.
-
Libya yatoa leseni za kwanza za mafuta kwa makampuni ya nishati ya nje tangu kupinduliwa Gaddafi
Feb 12, 2026 07:51Libya imetoa leseni kwa ajili ya uchimbaji na uzalishaji mafuta kwa makampuni kadhaa za nishati za kigeni, ikiwa ni pamoja na makampuni makubwa ya Chevron na BP kwa mara ya kwanza tangu kupinduliwa mamlakani kiongozi wa muda mrefu wa nchi hiyo Kanali Muammar Gaddafi.