-
Zarif: Masunni na Mashia lazima waungane kuzima ugaidi
Jul 24, 2016 00:00Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amelaani hujuma ya kigaidi ya hapo jana iliyosababisha vifo vya makumi ya watu nchini Afghanistan na kusisitiza kuwa, wakati umefika kwa Waislamu wa madhehebu ya Shia na Sunni waungane kwa shabaha ya kulikabili kwa pamoja jinamizi la ugaidi.
-
Rouhani: Ugaidi ni tishio kwa dunia nzima
Jul 06, 2016 00:02Rais Hassan Rouhani wa Iran ametoa mkono wa kheri na nafaka kwa kuwadia sherehe za Idul-Fitri na kumalizika mwezi mtukufu wa Ramadhani kwa marais wa nchi za Kiislamu na kusema kuwa, jinamizi la ugaidi ni tishio sio tu kwa nchi jirani na marafiki wa Jamhuri ya Kiislamu katika eneo hili Mashariki ya Kati, bali kote duniani.
-
Iran yakosoa ukosefu wa misaada ya kimataifa kwa wakimbizi Waafghani nchini
Jun 18, 2016 23:43Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Mohammad Javad Zarif ameikosoa jamii ya kimataifa kwa kutotoa misaada ya kutosha kwa ajili ya wakimbizi wa Afghanistan walioko nchini. Aidha amesisistiza kuhusu umuhimu wa kuandaa mazingira ya wakimbizi hao kurejeshwa kwa hiari nchini Afghanistan.
-
Hujuma ya kigaidi msikitini Afghanistan, wanne wauawa
Jun 10, 2016 23:16Watu wanne wameuawa na wengine wengi kujeruhiwa wakati magaidi walipoulenga msikiti kwa bomu katika mkoa wa Nangarhar mashariki mwa Afghanistan.
-
Raia wa Afghanistan aachiliwa huru kutoka jela ya Guantamano baada ya miaka 14
May 21, 2016 02:55Wizara ya Ulinzi ya Marekani imetangaza kuwa, tume ya kuchunguza faili za msamaha katika jela ya Guantanamo, imetoa amri ya kuachiliwa huru Ubaidullah, raia wa Afghanistan ambaye amekuwa akizuiliwa ndani ya jela hiyo ya kuogofya kwa miaka 14 sasa.
-
Pentagon: Hujuma ya US dhidi ya hospitali Afghanistan sio jinai ya kivita
Apr 30, 2016 03:14Wizara ya Ulinzi ya Marekani (Pentagon) imetetea mashambulizi ya anga yaliyofanywa na jeshi lake dhidi ya hospitali moja nchini Afghanistan mwishoni mwa mwaka jana 2015.
-
Makumi wauawa katika shambulizi la bomu Kabul, Afghanistan
Apr 19, 2016 03:26Makumi ya watu wameuawa na mamia ya wengine kujeruhiwa katika mripuko wa bomu ulioutikisa mji wa Kabul karibu na ubalozi wa Marekani nchini Afghanistan mapema leo.
-
Mafuriko yaua watu wasiopungua 38 Afghanistan
Apr 18, 2016 22:40Watu wasiopungua 38 wamefariki dunia kutokana na mafuriko yaliyosababishwa na mvua kali iliyonyesha maeneo ya kaskazini mwa Afghanistan.
-
Magaidi wa Taliban waendelea kupata himaya ya nchi za Magharibi
Mar 17, 2016 04:51Balozi wa Uingereza nchini Afghanistan, Dominic Jermey amesema kuwa nchi yake inao uhusiano wa karibu na kundi la kigaidi la Taliban na kwamba ikiwa serikali ya Kabul itahitajia, basi nchi yake inaweza kuutumia uhusiano huo kwa ajili ya kurejesha usalama na amani nchini humo.
-
Mafanikio ya jeshi la Afghanistan dhidi ya kundi la Daesh
Feb 22, 2016 00:10Sambamba na sisitizo la viongozi wa serikali ya Afghanistan katika kukabiliana na magaidi, makamanda wa jeshi wametangaza kusambaratisha ngome kuu ya kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh katika wilaya ya Achin mkoani Nangarhar, mashariki mwa nchi hiyo.