-
Utumwa, ukoloni; Ghana yataka nchi za AU kuunga mkono Azimio la Algiers
Feb 16, 2026 10:14Rais wa Ghana ametoa wito kwa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) kuunga mkono rasimu ya azimio lenye lengo la kutambua dhulma za kihistoria zilizosababishwa na biashara ya utumwa wa kuvuka Atlantiki.
-
Waziri Mkuu wa Ethiopia ahimiza kuwepo uhusiano wa heshima kati ya Afrika na Italia
Feb 15, 2026 07:56Abiy Ahmed Waziri Mkuu wa Ethiopia amehimiza kuhusu ushirikiano mpya kati ya Afrika na Ulaya unaozingatia utu na ustawi wa pamoja. Waziri Mkuu wa Ethiopia ameeleza haya alipokuwa mwenyeji wa Mkutano wa Pili wa Italia na Afrika mjini Addis Ababa mji mkuu wa nchi hiyo.
-
Katibu Mkuu wa UN: Lazima Afrika iwe na sauti na iweze kunufaika na rasilimali zake
Feb 14, 2026 09:56Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, ametoa wito mkali wa kuhakikisha haki na mageuzi yanatekelezwa na kuimarishwa ushirikiano wa kimataifa, huku akiutaja Umoja wa Afrika AU, kama “kinara wa ushirikiano wa kimataifa katika dunia iliyogawanyika”.
-
Rais Xi Jinping wa China: Tutaziondolea ushuru nchi za Afrika ifikapo mwezi Mei
Feb 14, 2026 09:55Rais Xi Jinping wa China ametangaza kuwa, nchi yake itaziondolea ushuru nchi zingine za Afrika ifikapo mwezi Mei mwaka huu.
-
Mradi wa Mauaji ya Kimbari wa Italia nchini Libya
Feb 07, 2026 02:37Karne ya ishirini Miladia haikushuhudia tu matukio ya kushangaza ya binadamu, bali pia ilibeba baadhi ya kurasa zenye giza kuu katika historia ya mwanadamu. Katika moyo wa bara la Afrika, nchini Libya, dola moja ya kikoloni kutoka Ulaya ilitekeleza mpango wa kishetani na uliopangwa kwa umakini kwa lengo la kuangamiza taifa zima.
-
Jeshi la Nigeria lawakomboa mateka 62 na kuwaua wanamgambo 2 kaskazini magharibi mwa nchi
Jan 22, 2026 03:08Jeshi la Nigeria limeripoti kuwa wanajeshi watano na afisa mmoja wa polisi wameuawa katika shambulizi la kuvizia kaskazini magharibi mwa nchi hiyo.
-
Afrika yakosoa hatua ya Trump ya kuiondoa US katika taasisi za kimataifa
Jan 14, 2026 06:45Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AU), Mahmoud Ali Youssouf ametoa wito wa kuimarishwa mifumo ya pande nyingi ili kushughulikia changamoto za kimataifa, siku chache baada ya Marekani kuchukua uamuzi wa upande mmoja wa kujiondoa katika taasisi mbalimbali za kimataifa.
-
SWAPO yaitaka Marekani imuachie Maduro bila masharti yoyote
Jan 08, 2026 06:28Chama tawala nchini Namibia cha South West Africa People's Organization (SWAPO), kimetoa wito wa kuachiliwa huru mara moja na bila masharti yoyote Rais wa Venezuela, Nicolas Maduro na mkewe.
-
Safari ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Israel huko Somaliland; Tel Aviv katika njia ya kuyumbisha amani Pembe ya Afrika
Jan 08, 2026 03:02Waziri wa Mambo ya Nje wa Israel amefanya safari huko Hargeisa, mji mkuu wa eneo la Somaliland, akiongoza ujumbe rasmi wa Israel.
-
Afrika yasisitiza mshikamano na Venezuela baada ya uvamizi wa Marekani kumteka nyara Maduro
Jan 07, 2026 08:04Nchi za Kiafrika zimesisitiza mshikamano wao na Venezuela kufuatia uvamizi uliofanywa na Marekani nchinii humo na kumteka nyara Rais Nicolas Maduro.