-
Russia: Kwa mtazamo wa mkuu wa UNICEF watoto wa Ghaza si muhimu kama wenzao wa Ukraine
Jan 25, 2025 02:42Balozi wa Russia katika Umoja wa Mataifa amemshutumu mkuu wa UNICEF kwa kuwapa kipaumbele watoto wa Ukraine kuliko watoto wenzao wa Ghaza baada ya kushindwa kulieleza Baraza la Usalama la umoja huo kuhusu masaibu ya watoto hao kama alivyofanya kwa watoto wa Ukraine.
-
Nchi za Magharibi zina nafasi gani katika kuongezeka ugaidi Afrika?
Jan 22, 2025 23:18Kuongezeka kwa shughuli za kigaidi katika maeneo mbalimbali ya Afrika kumegeuka kuwa tatizo kubwa katika bara hilo na pia katika mataifa mengi duniani. Hivi sasa, makundi kadhaa ya kigaidi yanaendesha shughuli zao katika maeneo tofauti ya Afrika.
-
UN: Mapambano dhidi ya ugaidi barani Afrika yaheshimu haki za binadamu
Jan 22, 2025 10:03Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa, mapambano ya kukabiliana kikamilifu na ugaidi barani Afrika yanapaswa kuhusisha uvumbuzi na mtazamo unaoheshimu haki za binadamu na utawala wa sheria.
-
Ghalibaf: Changamoto ya uhusiano wa kiuchumi wa Iran na Afrika ni usafiri
Jan 17, 2025 03:51Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) ameyataja matatizo ya usafiri kuwa ni miongoni mwa changamoto kubwa katika kupanua uhusiano wa kiuchumi wa Iran na bara la Afrika akisema: Uwezo wa kimataifa kama wa kundi la BRICS na Shanghai ni fursa muhimu za kustawisha ushirikiano wa kiuchumi.
-
Viongozi wa Afrika wasisitiza ushirikiano katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi
Jan 16, 2025 07:36Viongozi wa nchi za Kiafrika wamesisitiza udharura wa kushirikiana nchi za bara hilo na kubuni tekolojia ya kukabiliana na athari mbaya za mabadiliko ya tabianchi ili kuhakikisha bara la Afrika linapata maendeleo endelevu.
-
Besigye kushtakiwa katika Mahakama ya Kijeshi Uganda kwa kosa la uhaini lenye hukumu ya kifo
Jan 14, 2025 23:16Mahakama ya Kijeshi ya Uganda imetangaza kuwa, kiongozi mashuhuri wa upinzani nchini humo Daktari Kizza Besigye atafikishwa mahakamani kujibu shtaka zito la uhaini, ambalo linamuongezea matatizo ya kisheria mwanasiasa huyo kuelekea uchaguzi wa rais uliopangwa kufanyika 2026.
-
Chad yakosoa ubabe na ukoloni wa Ufaransa
Jan 08, 2025 12:07Kufuatia kauli za Rais wa Ufaransa kwamba nchi za Afrika zimesahau kuishukuru Paris kwa kushiriki katika kile anachosema ni 'mapambano dhidi ya ugaidi' katika eneo la Sahel, Waziri wa Mambo ya Nje wa Chad amekosoa maneno hayo na kuyalaani.
-
Chad na Senegal zakerwa na matamshi ya Rais wa Ufaransa dhidi ya viongozi wa Afrika
Jan 07, 2025 08:48Chad imeelezwa kukerwa na kauli iliyotolewa na Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron dhidi ya viongozi wa Afrika.
-
Ghana yafuta viza ya kuingia nchini humo kwa wenye pasi za kusafiria za Afrika
Jan 04, 2025 03:53Rais wa Ghana anayeondoka madarakani, Nana Akufo-Addo, ametangaza kuondoa viza ya kuingia nchini humo kwa wale wote wenye pasi za kusafria za Afrika.
-
Rais wa Kenya akiri hadharani: Vyombo vya usalama vimejichukulia mamlaka kinyume cha sheria
Jan 02, 2025 03:18Rais William Ruto wa Kenya kwa mara ya kwanza amekiri hadharani matumizi mabaya ya mamlaka yanayofanywa na vikosi vya usalama, kufuatia wimbi la utekaji nyara wenye utata ambao umezua maandamano makubwa ya upinzani nchini humo.