Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limelaani vikali shambulio dhidi ya askari jeshi wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati lililosababisha mauti ya mwanajeshi mmoja raia wa Rwanda na kujeruhi wengine wanane.
Duru za usalama za Jamhuri ya Afrika ya Kati zimetangaza habari ya kutokea mapigano baina ya watu wenye silaha na askari wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa karibu na Ikulu ya Rais mjini Bangui.
Duru za habari za Jamhuri ya Afrika ya Kati zimeripoti kuwa, kumezuka mapigano mapya kati ya makundi ya wabeba silaha na kupelekea watu kadhaa kuuawa, katika maeneo ya kaskazini magharibi mwa nchi hiyo.
Wanajeshi wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati wameripoti kuwa watu wawili wameuawa na wawili wengine kujeruhiwa katika mapigano yaliyotokea baina ya watu wenye silaha kusini mwa nchi hiyo.
Mahakama moja nchini Ufaransa imetangaza kuhitimisha faili la tuhuma za askari wa nchi hiyo waliowanajisi watoto wa Jamhuri ya Afrika ya Kati kwa madai ya kutokuwepo ushahidi wa kutosha.
Nusu ya raia wa Jamhuri ya Afrika ya Kati wanahitajia misaada ya kibinadamu huku kukitolewa miito ya kuwasaidia haraka raia hao.
Wapiganaji wa kundi la Kikristo la Anti barala wameua askari mmoja wa kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Mataifa katika Jamhuri ya Afrika ya Kati na kujeruhi wengine watatu.
Duru za habari zinaripoti kutoka katika Jamhuri ya Afrika ya Kati kwamba, mapigano makali yamezuka tena katika nchi hiyo na kuzusha wasiwasi mkubwa miongoni mwa raia.
Jumuiya ya Madaktari Wasio na Mipaka (MSF) imeripoti kuwa mapigano makali yangali yanaendelea katika mkoa wa Ouham kaskazini mwa Jamhuri ya Afrika ya Kati.
Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) na taasisi ya al Azhar nchini Misri zimelaani mauaji yanayofanywa dhidi ya Waislamu katika Jamhuri ya Afrika ya Kati.