-
Mivutano baina ya Marekani na China yashadidi baada ya hotuba ya Trump katika Umoja wa Mataifa
Sep 24, 2020 04:40Katika hotuba yake ya mwisho kwenye ukumbi wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa katika kipindi chake cha kwanza cha urais wa Marekani, Donald Trump amejikita zaidi katika masuala ya China na Iran na kudai kuwa, Marekani imejiondoa katika makubaliano mabaya sana ya nyuklia ya JCPOA na imeiwekea Iran vikwazo vya kulema.
-
Msimamo mmoja wa kundi la 4+1 mbele ya madai hewa ya Marekani kuhusu Iran
Sep 21, 2020 07:03Licha ya Marekani kutoa madai hewa ya kuanza kutekelezwa vikwazo vya kimataifa dhidi ya Iran kuanzia jana Jumapili Septemba 20, 2020 vikiwemo vikwazo vya silaha, lakini mataifa ya dunia yamepinga madai hayo ya Washington na yamechukua msimamo imara kiasi kwamba inaonekana kama vile hakuna mabadiliko yoyote yaliyotokea.
-
Taiwan; mstari mwekundu wa China
Sep 19, 2020 02:19Ijumaa ya jana tarehe 18 Septemba, jeshi la China lilianza kufanya luteka ya kijeshi jirani na Taiwan katika kipindi hiki cha anga ya mzozo na mvutano baina ya Beijing na Taipei.
-
Lavrov apinga tuhuma kwamba Russia inaingilia uchaguzi wa Marekani
Sep 13, 2020 03:04Uhusiano wa Russia na Marekani umekuwa na mivutano mikubwa baada ya kutokea mgogoro huko Ukraine mwaka 2014. Moja ya kadhia ambazo zimebadilika huko Marekani katika miaka ya karibuni na kuwa dhidi ya Moscow ni mjadala wa madai ya Russia kuingilia uchaguzi wa Marekani. Kwa kuzingatia kukaribia kufanyika uchaguzi wa Rais wa Marekani hivi sasa soko la tuhuma hizo limezidi kupamba moto.
-
Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran: Tehran haijali nani atakua rais wa Marekani, Trump au Biden
Sep 11, 2020 06:25Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Iran amesema kuwa si suala muhimu mwa Tehran kujua nani atakuwa rais wa Marekani na kuongeza kuwa, katika kipindi chote cha miongo minne iliyopita Marekani imekuwa ikiingilia chaguzi zinazofanyika katika nchi mblimbali duniani.
-
Makabiliano ya Marekani na China Mashariki mwa Asia
Sep 05, 2020 06:38Waziri wa Mambo ya Nje wa China amewatolea wito wanachama wa Jumuiya ya Nchi za Kusini Mashariki mwa Asia (ASEAN) kuendelea kupinga uingiliaji wa Marekani katika eneo hilo.
-
Russia na China zapongeza kikao cha Kamisheni ya Pamoja ya JCPOA
Sep 02, 2020 03:31Russia na China zimepongeza mkutano wa Kamisheni ya Pamoja ya JCPOA uliofanyika jana Jumanne huko Vienna, mji mkuu wa Austria.
-
China yaonya: Ikilazimu, tutaingia katika makabiliano ya kijeshi na Marekani
Aug 29, 2020 19:31Jeshi la China limetahadharisha kuwa, huenda litalazimika kuingia katika makabiliano ya kijeshi na Marekani pasi na kukusudia iwapo Washington haitasitisha operesheni zake za kichokozi katika Bahari ya Kusini ya China.
-
Kuumbuka tena Marekani kwa kukataliwa takwa lake la kutekeleza "Snapback Mechanism" na Rais wa Baraza la Usalama la UN
Aug 26, 2020 08:18Baada ya Marekani kugonga mwamba kwa kushindwa kufanikisha njama yake ya kurefusha vikwazo vya silaha dhidi ya Iran kupitia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, iliamua kuwasilisha shtaka jengine dhidi ya Tehran kwa kisingizio kuwa eti imekiuka msingi wa makubaliano ya nyuklia ya JCPOA na kwa hivyo ikataka utekelezwe Utaratibu wa Kurejesha Vikwazo Papo kwa Papo, unaojulikana kitaalamu kama 'Snapback Mechanism';
-
Kampuni ya TikTok ya China kumshtaki Rais Trump wa Marekani
Aug 25, 2020 22:18Kampuni ya TikTok ya China imefungua kesi ya kupinga amri ya Rais Donal Trump wa Marekani inayozuia shughuli zozote za kampuni mama ya kampuni ,ByteDance, kuendesha shughuli zake nchini Marekani.