-
Kituo cha Kiislamu chachomwa moto Marekani siku ya kwanza ya Ramadhani
Apr 26, 2020 07:55Baraza la Uhusiano wa Kiislamu nchini Marekani (CAIR) limezitaka mamlaka husika nchini humo kuchunguza kitendo cha kuteketezwa kwa moto Kituo cha Kiislamu katika jimbo la Missouri, katika siku ya kwanza ya mwezi mtukufu wa Ramadhani.
-
Indhari ya Katibu Mkuu wa UN kuhusu uenezaji hofu na chuki dhidi ya Uislamu duniani
Feb 18, 2020 08:13Kujitokeza makundi ya kigaidi na yenye misimamo ya kufurutu mpaka na kuenea katika nchi za Magharibi vitendo vya kigaidi vinavyofanywa na makundi hayo, na vile vile kujitokeza mgogoro wa wakimbizi, ambao akthari yao ni Waislamu, yote hayo yametumiwa na baadhi ya viongozi na vyombo vya habari vya Magharibi kama kisingizio cha kueneza hofu na chuki dhidi ya Uislamu; jambo ambalo limeufanya Umoja wa Mataifa ulazimike kupaza sauti yake.
-
Guterres abainisha wasiwasi wake kuhusu kuongezeka chuki dhidi ya Uislamu duniani
Feb 17, 2020 07:48Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa anatiwa wasiwasi na kuongezeka vitendo vya chuki dhidi ya Uislamu duniani na akasema mwenendo huo hauvumiliki.
-
Maelfu ya Waislamu waandamana Ufaransa kupinga chuki dhidi ya Uislamu
Nov 11, 2019 12:48Maelfu ya watu wameshiriki maandamano katika mji mkuu wa Ufaransa, Paris kulalamikia chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu nchini humo.
-
Shambulizi dhidi ya msikiti Ufaransa; watu wawili wapigwa risasi
Oct 29, 2019 03:41Watu wawili wamejeruhiwa vibaya baada ya kupigwa risasi nje ya msikiti mmoja katika mji wa Bayonne, kusini magharibi mwa Ufaransa.
-
Mwanafunzi wa Kiislamu Marekani aondolewa mashindanoni kwa kuvaa hijabu
Oct 26, 2019 11:54Mwanafunzi wa kike wa shule moja katika jimbo la Ohio nchini Marekani ameondolewa kwenye mashindano ya mbio za nyika kwa kuvaa vazi la stara la hijabu.
-
Boris Johnson aushutumu Uislamu kuwa umezuia maendeleo katika baadhi ya maeneo duniani
Jul 16, 2019 12:03Mgombea anayeongoza katika kinyang'anyiro cha uwaziri mkuu wa Uingereza ametoa matamshi ya kuushutumu Uislamu kwa kudai kuwa dini hiyo ya Mwenyezi Mungu inazuia kupatikana ustawi na maendeleo katika jamii.
-
Waziri Mkuu wa Pakistan: Umma upambane na chuki dhidi ya Uislamu
Jun 01, 2019 11:25Waziri Mkuu wa Pakistan Imran Khan ametoa mwito kwa umma wa Kiislamu kupambana na dhulma na chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu duniani.
-
CAIR yaonya kuhusu kuenea chuki dhidi ya Uislamu baada ya mbunge Muislamu kutishiwa kuuawa Marekani
Apr 07, 2019 02:59Baraza la Uhusiano wa Kiislamu nchini Marekani (CAIR) limeonya kuwa vitendo vya uhalifu vinavyotokana na chuki dhidi ya Waislamu vimeongezeka nchini humo, baada ya mtu mmoja kukamatwa na kupandishwa kizimbani kwa kutishia kumuua Mbunge Muislamu katika Baraza la Wawakilishi la Marekani, Ilhan Omar.
-
Bunge la Australia lamjia juu Seneta mwenye chuki dhidi ya Waislamu
Apr 04, 2019 02:35Bunge la Australia limepiga kura kwa kishindo kupasisha hoja ya kumlaani na kumkosoa Seneta mwenye misimamo mikali wa mrengo wa kulia, kutokana na matamshi yake ya chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu baada ya shambulizi la kigaidi la mwezi uliopita nchini New Zealand.