-
Qassemi: Zama za kutumia vitisho vya kijeshi zimepita
Aug 14, 2017 04:22Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amekosoa vitisho vya kutumia nguvu za jeshi vilivyotolewa na Rais Donald Trump wa Marekani dhidi ya Venezuela na kusisitiza kuwa uzoefu unaonesha kuwa, zama za kutumia vitisho vya kijeshi na mashinikizo dhidi ya nchi huru na zinazojitawala kwa ajili ya kuzilazimisha zikubali matakwa yasiyo ya kimantiki na haramu zimemalizika.
-
Araqchi: Hatua ya Kongresi ya Marekani ni mwendelezo wa uadui wa Washington dhidi ya Iran
Jul 30, 2017 03:26Mkuu wa timu ya Iran ya kufuatilia utekelezwaji wa makubaliano ya nyuklia yanayojulikana kama Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji (JCPOA) amesema kuwa, hatua ya hivi karibuni ya Kongresi ya Marekani ya kupasisha vikwazo vipya dhidi ya Iran ni hatua ya kiuadui na chuki dhidi ya Tehran.
-
New York Times: Trump anafanya njama za kuionyesha Iran kuwa ndio iliyokiuka JCPOA
Jul 28, 2017 21:52Mchambuzi wa masuala ya kisiasa na mhariri wa gazeti la The New York Times amesema kuwa, Rais Donald Trump wa Marekani, anafanya njama za kuionyesha Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kuwa ndiyo iliyokiuka makubaliano ya nyuklia yanayojulikana kwa kifupi kama JCPOA.
-
Kuongezeka mpasuko ndani ya serikali ya Rais Donald Trump wa Marekani
Jul 23, 2017 06:44Katika hatua mpya inayodhihirisha mpasuko uliopo ndani ya serikali ya Rais Donald Trump wa Marekani, Sean Spicer Msemaji wa Ikulu ya Rais wa nchi hiyo (White House) ametangaza kujiuzulu wadhifa wake.
-
Gazeti la The Guardian: Trump anaelekea kuisambaratisha Marekani
Jul 21, 2017 03:39Gazeti la The Guardian linalochapishwa mjini London, Uingereza limeandika kuwa, hatua za Rais Donald Trump wa Marekani zinaisambaratisha nchi hiyo.
-
Trump kumaliza ushirikiano wa CIA na magaidi wa Syria
Jul 20, 2017 03:21Serikali ya rais wa Marekani, Donald Trump imeamua kumaliza miaka kadhaa ya ushirikiano wa Shirika la Kijasusi la Marekani CIA na magenge ya kigaidi nchini Syria ambayo Wamarekani wanadai ni wapinzani wenye misimamo ya wastani wanaopigana na serikali ya Rais Bashar al Assad. Shirika la Kijasusi la Marekani limekuwa likiyapa silaha na mafunzo ya kijeshi magenge hayo kwa miaka kadhaa sasa.
-
Wacanada waandamana kupinga ziara ya familia ya Trump katika mji wa Vancouver
Jul 13, 2017 03:51Wakazi wa mji wa Vancouver, Canada wamefanya maandamano makubwa kupinga ziara ya familia ya Rais Donald Trump wa Marekani katika mji huo.
-
Trump akosolewa kwa mahudhurio dhaifu mkutano wa G20, Hamburg
Jul 10, 2017 02:44Duru za Marekani zimekosoa mahudhurio dhaifu na mienendo ya Rais Donald Trump wa nchi hiyo katika mkutano uliomalizika juzi wa viongozi wa nchi za G20 nchini Ujerumani.
-
Matokeo ya mazungumzo ya Trump na Putin mjini Hamburg Ujerumaini
Jul 09, 2017 03:30Baada ya kupita miezi mingi ya malalamiko ya Wamarekani kwa Russia wanaodai kuwa Moscow inaingilia masuala ya ndani ya nchi yao, hatimaye marais wawili wa nchi hizo mbili wamekutana pambizoni mwa kikao cha viongozi wa G20 mjini Hamburg, Ujerumani. Hayo yalikuwa ni mazungumzo ya kwanza ya marais hao wawili tangu Donald Trump atangazwe kuwa rais wa Marekani.
-
Trump: Ni lazima China ichukue hatua kali dhidi ya Korea Kaskazini
Jul 04, 2017 03:45Rais Donald Trump wa Marekani ameitaka Uchina kuchukua uamuzi mgumu kuhusiana na hatua ya Pyongyang ya kuvurumisha kombora jipya la balestiki mapema leo.