Apr 05, 2018 01:37
Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, juhudi za pande tatu za Iran, Uturuki na Russia zimepelekea Syria kupata mafanikkio makubwa katika vita dhidi ya magaidi na kwamba, kuna haja ya juhudi hizo kuendelezwa hadi pale wananchi wa nchi hiyo ya Kiarabu watakapoweza kuishi katika mazingira tulivu na ya amani kamili.