-
Umoja wa Mataifa kuchunguza jinai za kivita huko Tigray
Nov 03, 2021 08:34Umoja wa Mataifa umeamua kufanya uchunguzi na kutoa ripoti kuhusu jinai za kutisha zinazoripotiwa kufanyika katika eneo la Tigray huko kaskazini mw Ethiopia.
-
Wakazi wa Addis Ababa watakiwa kuulinda mji huo baada ya waasi wa Tigray kusonga mbele
Nov 03, 2021 00:02Mamlaka za mji mkuu wa Ethiopia, Addis Ababa zimetoa wito kwa wakaazi wa mji huo kujiandaa kutetea vitongoji vyao baada ya vikosi vya waasi kutoka eneo la Tigray, ambao wamekuwa wakipigana na serikali kuu kwa mwaka mmoja sasa, kuashiria kwamba huenda wakasonga mbele kuelekea kwenye mji huo.
-
Waasi wa harakati ya TPLF wadai kuteka mji wa kistratijia wa Dessie, Ethiopia
Oct 31, 2021 03:44Wapiganaji wa kundi la waasi wa harakati ya Ukombozi wa Watu wa Tigray (TPLF) wamedai kuwa wamefanikiwa kuteka kikamilifu mji wa kistratijia wa Dessie ulioko katika jimbo la Amhara huko kaskazini mwa Ethiopia.
-
Watoto 3 wauawa katika shambulio la anga Ethiopia
Oct 19, 2021 10:03Umoja wa Mataifa umesema watoto watatu wameuawa huku mtu mmoja akijeruhiwa katika shambulio la anga lililolenga eneo la Mekelle, makao makuu ya eneo la Tigray kaskaizni mwa Ethiopia.
-
Mapigano mapya yashtadi eneo la Tigray, kaskazini mwa Ethiopia
Oct 13, 2021 09:27Duru za kiusalama zimearifu kuwa, mapigano makali yamechachamaa katika eneo la Tigray la kaskazini mwa Ethiopia baina ya wanajeshi wa serikali ya Addis Ababa na wapiganaji wa Harakati ya Ukombozi wa Watu wa Tigray (TPLF).
-
Abiy aapishwa kuongoza muhula wa pili nchini Ethiopia
Oct 04, 2021 08:08Waziri Mkuu wa Ethiopia, Abiy Ahmed ameapishwa leo Jumatatu kuongoza muhula mpya wa miaka mitano katika nchi hiyo ya Pembe ya Afrika inayokabiliwa na uasi na mapigano ya kikabila.
-
Katibu Mkuu wa UN: Nimeshtushwa na hatua ya Ethiopia kuwatimua maafisa wetu
Oct 01, 2021 09:56Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema ameshtushwa sana na kitendo cha serikali ya Ethiopia kuwafukuza maafisa wa umoja huo wanaohudumu nchini humo.
-
Serikali ya Ethiopia yatoa amri ya kutimuliwa maafisa 7 wa UN kwa "kuingilia" masuala ya ndani ya nchi hiyo
Sep 30, 2021 22:57Serikali ya Ethiopia imeamuru maafisa saba waandamizi wa Umoja wa Mataifa waondolewe nchini humo kwa kile ilichokiita kuingilia masuala ya ndani ya nchi hiyo.
-
UN: Mamia ya malori ya misaada ya kibinadamu yanazuiliwa Tigray
Sep 17, 2021 21:59Mamia ya malori ya misaada ya kibinadamu yanazuiliwa kutoka katika eneo lililoathiriwa na mapigano la Tigray kaskazini mwa Ethiopia, na kutoonekana kwa malori hayo kunatajwa kuwa ndiyo sababu kuu ya kupungua kwa misaada ya kibindamu. Hayo yamesemwa na Umoja wa Mataifa.
-
Raia 125 wauawa katika hujuma ya waasi kaskazini mwa Ethiopia
Sep 09, 2021 05:19Madaktari wa Ethiopia wamethibitisha kuwa raia wasiopungua 125 wameuawa katika shambulizi lililofanywa na wapiganaji wa kundi la TPLF huko kaskazini mwa nchi hiyo.