Sep 11, 2018 13:54
Mashirika ya kutetea haki za binadamu yameikosoa vikali Marekani kwa kuishambulia na kutishia kuiwekea vikwazo Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC, baada ya korti hiyo yenye makao yake mjini The Hague nchini Uholanzi kusema kuwa itawafungulia mashitaka wanajeshi wa Marekani waliohusika katika jinai za kivita nchini Afghanistan.