-
Marekani yakosolewa kwa kuitolea vitisho mahakama ya ICC
Sep 11, 2018 09:24Mashirika ya kutetea haki za binadamu yameikosoa vikali Marekani kwa kuishambulia na kutishia kuiwekea vikwazo Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC, baada ya korti hiyo yenye makao yake mjini The Hague nchini Uholanzi kusema kuwa itawafungulia mashitaka wanajeshi wa Marekani waliohusika katika jinai za kivita nchini Afghanistan.
-
Kamishna wa Haki za Binadamu wa UN: Wanachama wa kudumu wa Baraza la Usalama hawakuniunga mkono
Aug 17, 2018 23:44Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa anayemaliza muda wake amesema hana hamu ya kuendelea kuhudumu katika wadhifa huo kutokana na kukosa uungaji mkono wa nchi tano wanachama wa kudumu wa Baraza la Usalama la umoja huo kwa taasisi aliyokuwa akiiongoza.
-
AI: Kutenganisha watoto wa wahajiri na wazazi wao Marekani ni jinai mbaya zaidi duniani
Aug 16, 2018 22:52Mkurugenzi Mkuu mpya wa shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International (AI) amesema kuwa, hatua iliyochukuliwa na serikali ya Rais Donald Trump wa Marekani ya kuwatenganisha watoto wadogo na wazazi wao wahajiri ni miongoni mwa jinai mbaya zaidi zilizowahi kushuhudiwa duniani.
-
Michelle Bachelet aidhinishwa rasmi kuwa Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu UN
Aug 11, 2018 03:11Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limemuidhinisha rais wa zamani wa Chile Michelle Bachelet kuwa Kamishna Mkuu mpya wa Haki za Binadamu wa umoja huo.
-
Kongamano la Tatu la Haki za Binadamu kwa Mtazamo wa Kiislamu laanza Tehran
Aug 04, 2018 03:44Kongamano la Tatu la Kimataifa la Haki za Binadamu za Kiislamu limeanza leo katika mji mkuu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Tehran.
-
UN yaeleza wasiwasi wake kuhusu ukiukwaji wa haki za binadamu Saudia
Jul 31, 2018 10:02Umoja wa Mataifa umeeleza wasiwasi wake kuhusu mwenendo wa kuendelea kukamatwa wapinzani wa serikali nchini Saudi Arabia.
-
Mpango wa jeshi la Myanmar wa kuwaua Waislamu wa Rohingya
Jul 20, 2018 03:11Shirika la kutetea haki za binadamu la eneo la Asia, limetangaza kwamba ukatili na mauaji dhidi ya Waislamu wa Rohingya yaliyofanywa na jeshi la Myanmar yaliratibiwa mapema na kutekelezwa kwa mpangilio maalumu.
-
Ayatullah Amoli Larijani: Ni Jukumu la Waislamu kuonyesha sura khabithi ya Marekani
Jul 03, 2018 00:25Mkuu wa Vyombo vya Mahakama nchini Iran ameashiria jinai za Marekani nchini Iran na Yemen na kujitoa serikali ya Rais Donald Trump katika Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa na kusema kuwa, hatua za serikali ya Washington ni za kibabe.
-
Human Rights Watch yakosoa sera za Donald Trump
Jun 30, 2018 03:21Shirika la Kutetea Haki za Binadamu la Human Rights Watch limekosoa vikali sera za hivi karibuni za serikali ya Rais Donald Trump wa Marekani.
-
Mashirika 20 ya kimataifa yaandika barua kupinga madai ya Marekani kuhusu Baraza la Haki za Binadamu
Jun 25, 2018 10:12Mashirika 20 ya kimataifa yasiyo ya kiserikali yamepinga madai ya Marekani kuhusu sababu zilizoifanya Washington ijitoe katika Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa na yametetea utendaji wa baraza hilo.