Jun 12, 2018 13:50
Qatar imewasilisha faili la kesi dhidi ya Umoja wa Falme za Kiarabu, katika mahakama ya juu zaidi ya Umoja wa Mataifa, ikiituhumu Abu Dhabi kwamba imekiuka haki za binadamu za wananchi wa Qatar, huku mgogoro wa nchi hizo za Kiarabu ukielekea kutimiza mwaka mmoja.