-
Katibu Mkuu wa UN atuma rambirambi kufuatia kufa shahidi Ebrahim Raisi na wenzake
May 21, 2024 08:56Antonio Guterres Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametuma salamu za rambirambi kwa familia za shahidi Rais Sayyid Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wenzake aliokuwa amefuatana nao na kutoa mkono wa pole kwa serikali na wananchi wa Iran.
-
Kaimu Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran aarifishwa rasmi Umoja wa Mataifa
May 21, 2024 08:51Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa wa Mataifa katika barua rasmi kwa Umoja wa Mataifa amewaarifisha katika taasisi hiyo ya kimataifa Kaimu Rais na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran kuwa viongozi wa muda katika nyadhifa hizo.
-
Iran yatangaza tarehe ya uchaguzi wa rais; Sayyid Raisi kuzikwa Alkhamisi
May 21, 2024 03:50Iran imetangaza Juni 28, 2024 kuwa tarehe ya kufanyika uchaguzi wa rais, kufuatia kufa shahidi Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu katika ajali ya helikopta iliyotokoea Jumapili katika mkoa wa Azarbaijan Mashariki, kaskazini magharibi mwa Iran.
-
Serikali: Uchaguzi wa rais wa Iran utafanyika ndani ya siku 50
May 20, 2024 04:19Msemaji wa Baraza la Kulinda Katiba ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema baraza maalumu litaundwa kwa ajili ya kuandaa mazingira ya kufanyika uchaguzi wa rais katika kipindi cha siku 50 zijazo.
-
Viongozi wa dunia wasikitishwa na kifo cha Rais wa Iran
May 20, 2024 03:54Viongozi wa mataifa mbali mbali duniani wameendelea kutoa mkono wa pole kufuatia vifo vya Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Sayyid Ebrahim Raisi pamoja na wenzake kadhaa katika ajali ya helikopta iliyotokea jana katika mkoa wa Azarbaijan Mashariki, kaskazini magharibi mwa Iran.
-
Rais Ebrahim Raisi na ujumbe aliofuatana nao, wafa shahidi katika ajali ya helikopta
May 20, 2024 02:10Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Seyed Ebrahim Raisi na viongozi kadhaa aliofuatana nao wamekufa shahidi katika ajali ya helikopta iliyotokea katika eneo la Varzghan mkoani Azerbaijan Mashariki wakiwa katika kazi ya kuwahudumia na kuwatumikia wananchi.
-
Imethibitishwa: Rais Ebrahim Raisi na wenzake wameaga dunia katika ajali ya helikopta
May 20, 2024 01:20Habari iliyotufikia hivi punde inasema kuwa, imethibitika kuwa Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Sayyid Ebrahim Raisi ameaga dunia akiwa na wenzake kadhaa katika ajali ya helikopta iliyotokea jana katika mkoa wa Azarbaijan Kashariki, kaskazini magharibi mwa Iran.
-
Iran yakanusha taarifa 'isiyokubalika' ya Arab League kuhusu visiwa vyake vitatu vilivyoko Ghuba ya Uajemi
May 18, 2024 23:16Nasser Kan’ani, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, amesisitiza kuwa visiwa vitatu vya Bu Musa na Tunb Kubwa na Ndogo vilivyoko katika Ghuba ya Uajemi vitaendelea kuwa sehemu isiyotenganishika ya ardhi ya Iran na kwamba madai yasiyo na msingi yanayotolewa na Jumuiya ya Nchi za Kiarabu kuhusu suala hilo hayakubaliki kabisa.
-
Iran yaikataa taarifa 'isiyokubalika' ya Arab League kuhusu visiwa vyake vitatu vilivyoko Ghuba ya Uajemi
May 17, 2024 04:49Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetupilia mbali kauli "isiyo na msingi" na "isiyokubalika" iliyotolewa na Jumuiya ya Nchi za Kiarabu kuhusiana na visiwa vitatu vya Abu Musa na Tunb Kubwa na Ndogo vilivyoko katika Ghuba ya Uajemi na kusisitiza kuwa visiwa hivyo vitabaki kuwa milki ya Iran.
-
"Mauaji ya watoto 15,000 wa Gaza yanaashiria mwisho wa Israel"
May 14, 2024 23:49Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema hakuna shaka kuwa mauaji ya watoto zaidi ya 15,000 wa Kipalestina katika Ukanda wa Gaza itakuwa chachu ya kuharakisha mchakato wa kuporomoka na kusambaratika utawala wa Kizayuni wa Israel.