-
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu: Njia ya kukomesha dhulma kubwa ya kuwepo utawala wa Kizayuni itaendelea
Mar 20, 2024 23:30Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran amesema: Njia ya kukomesha dhulma kubwa ya kuwepo utawala wa Kizayuni wa Israel itaendelea.
-
Iran yaonya kuhusu hatua za Wazayuni dhidi ya Wapalestina wanaokwenda kusali Msikiti wa Al-Aqsa
Mar 20, 2024 08:41Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametahadharisha kuhusu vitendo vyovyote vya kichokozi vinavyoweza kufanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel katika eneo la Quds Tukufu na Msikiti wa Al-Aqsa dhidi ya Waislamu Wapalestina wanaokwenda kusali katika msikiti huo wakati huu wa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.
-
Iran: Shutuma za USA na UK kuhusu Bahari Nyekundu na Yemen hazina msingi wowote
Mar 19, 2024 04:27Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amekanusha tuhuma zisizo na msingi za Marekani na Uingereza dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kuhusu hali ya Bahari Nyekundu na Yemen.
-
Abdollahian: Iran ina azma ya kuimarisha uhusiano na Niger
Mar 18, 2024 10:04Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesisitiza kuwa serikali ya Rais Ebrahim Raisi ina hamu ya kuimarisha zaidi uhusiano na ushirikiano na nchi za Afrika ikiwemo Niger.
-
Mashirika 16 ya Kiirani katika maonyesho ya afya Kenya
Mar 17, 2024 07:40Mashirika 16 ya ubunifu wa utaalamu ya Iran yanashiriki katika duru ya 24 la Maonyesho ya Sekta ya Afya nchini Kenya, yaliyopangwa kufanyika Nairobi kuanzia tarehe 17 hadi 19 mwezi Aprili mwaka huu.
-
Waziri wa Ulinzi: Iran iko tayari kuisaidia Syria kuimarisha nguvu zake za kiulinzi na za kuzuia mashambulio
Mar 17, 2024 02:28Waziri wa Ulinzi wa Iran Brigedia Jenerali Mohammad Reza Ashtiani amesema Jamhuri ya Kiislamu iko tayari kutumia uwezo wake wote kuisaidia Syria katika kuimarisha ulinzi na uwezo wake wa kuzuia hujuma za Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Kurefushwa hali ya hatari kitaifa; muendelezo wa mtazamo wa uadui wa Marekani dhidi ya Iran
Mar 14, 2024 23:17Siku ya Jumanne, Rais Joe Biden wa Marekani alirefusha kwa mwaka mwingine mmoja, muda wa hali ya hatari ya kitaifa kuhusu Iran. Tangu 1995, marais wote wa Marekani wamekuwa wakirefusha kila mwaka hali hiyo iliyoanza kutekelezwa kupitia Agizo la Utendaji nambari 12957 dhidi ya Iran.
-
Rais wa Iran asisitiza maendeleo katika uga wa sayansi na teknolojia
Mar 14, 2024 03:48Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema sayansi na teknoliojia ni kati ya maeneo ambayo maadui wanayatamani ili kuirudisha nyuma Iran ya Kiislamu na akasisitiza maendeleo katika uwanja huo.
-
Waziri wa Ulinzi : Iran imepiga hatua kubwa katika uzalishaji wa ndege zisizo na rubani (Droni)
Mar 13, 2024 23:06Waziri wa Ulinzi wa Iran Brigedia Jenerali Mohammad Reza Ashtiani amesema kuwa uuzaji nje wa zana za kijeshi umeongezeka pakubwa katika miaka ya karibuni.
-
Iran na Iraq zasisitizia haja ya kusimamishwa mauaji ya kimbari Gaza
Mar 13, 2024 04:16Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran na Iraq wametoa mwito wa kuchukua hatua zaidi hasa za kisiasa kwa ajili ya kusimamisha mauaji ya kimbari yanayofanywa na utawala wa Kizayuni dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza.