-
Raisi: Veto ya US katika Baraza la Usalama ni 'dhulma maradufu' kwa Wapalestina
Oct 19, 2023 11:41Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema hatua ya Marekani ya kulipigia kura ya turufu azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa linalotaka kusimamishwa mashambulizi na jinai za Israel dhidi ya wakazi wa Ukanda wa Gaza ni dhulma maradufu dhidi ya Wapalestina na ubinadamu.
-
Abdollahian alaani jinai za Israel Gaza: Muda wa utawala wa Kizayuni umemalizika
Oct 18, 2023 08:55Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameashiria kitendo cha Israel cha kushambulia kwa mabomu hospitali na shule katika Ukanda wa Gaza huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu na kueleza kuwa: Muda wa kubaki hai utawala wa Kizayuni umemalizika.
-
Abdollahian: Sera za Marekani zinachochea moto wa vita Gaza
Oct 17, 2023 10:05Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema sera haribifu za Washington na uungaji mkono wake kwa hatua ya utawala wa Kizayuni ya kuwashambulia raia katika Ukanda wa Gaza ndiyo sababu kuu ya kushadidi na kupanuka vita katika eneo hilo la pwani ambalo liko chini ya mzingiro.
-
Raisi: Inapasa kuwabebesha dhima wanaonyamazia kimya jinai za Israel
Oct 15, 2023 23:38Rais Ebrahim Raisi wa Iran amesema kuliunga mkono taifa linalodhulumiwa la Palestina ni katika misingi ya sera za Jamhuri ya Kiislamu na kuongeza kuwa, wanaonyamazia kimya jinai za Israel watabeba mas'ulia mbele ya Mwenyezi Mungu, mienendo yao na historia.
-
Iran yakosoa taarifa ya Arab League kuhusu Gaza
Oct 14, 2023 03:32Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema taarifa mpya ya Jumuiya ya Nchi za Kiarabu juu ya matukio ya Ukanda wa Gaza inakera na kufedhehesha.
-
Abdollahian na Nasrullah wazungumzia matukio ya karibuni kuhusu vita vya Gaza
Oct 13, 2023 23:58Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amekutana na kufanya mazungumzo na Sayyed Hassan Nasrallah, Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah Sayyed katika ziara yake nchini Lebanon.
-
Meja Jenerali Salami: Kimbunga cha Al-Aqswa ni ushindi mkubwa zaidi wa harakati ya Palestina
Oct 13, 2023 23:32Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (SEPAH) amesema kuwa, kipigo kikubwa zaidi katika historia ya uwepo wa utawala bandia wa Kizayuni tangu mwaka 1948 kwa utawala huo na ushindi mkubwa zaidi wa harakati ya Palestina ulitokea katika operesheni ya kimbunga ya Al-Aqswa.
-
Azimio la mwisho katika maandamano ya Iran ya kulaani jinai za utawala wa Kizayuni
Oct 13, 2023 08:30Washiriki wa maandamano ya leo hapa nchini ya kulaani jinai za utawala wa Kizayuni wamewasilisha azimio mwishoni mwa maandamano hayo na kutangaza uungaji mkono wao kwa wananchi madhlumu wa Palestina.
-
Safari ya kieneo ya Amir Abdollahian inayoangazia vita vya Gaza
Oct 13, 2023 08:07Huku utawala wa Kizayuni ukiendeleza hujuma na vita vyake vya jinai dhidi ya watu wasio na hatia wa Ukanda wa Gaza, Hossein Amirabdollahian, Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran anasisitiza ulazima wa kukomeshwa jinai hizo za Wazayuni kwa kufanya safari katika nchi kadhaa za eneo.
-
Iran yakanusha madai ya kuendelea kuzuiliwa fedha zake zilizoachiwa
Oct 13, 2023 03:44Ofisi ya Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa imekadhibisha ripoti iliyochapishwa na gazeti la Washington Post kuwa, Marekani na Qatar zimeafikiana kuzuia fedha za Iran zilizoachiwa hivi karibuni, ambazo zilikuwa zinashikiliwa nchini Korea Kusini kutokana na vikwazo.