-
Iran: Mapambano dhidi ya Israel yanaweza kuchukua mkondo mpana
Oct 13, 2023 00:02Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema mapambano dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel ambayo yameutumbukiza Ukanda wa Gaza katika vita haribifu na vya kuogofya, huenda yakachukua mikondo mipya na mipana zaidi.
-
Spika wa Iran azungumza na maspika wa nchi 7 za Kiislamu kuhusu jinai za Wazayuni Palestina
Oct 12, 2023 10:00Spika wa Majlisi ya Ushauri wa Kiislamu (Bunge la Iran) amefanya mazungumzo ya simu kwa nyakati tofauti na maspika wa mabunge ya nchi za Kiislamu za Uturuki, Algeria, Syria, Imarati, Lebanon, Oman na Kuwait na kuwahimiza wajibu wa kuchukuliwa hatua za haraka za kukomesha jinai za Wazayuni katika Ukanda wa Ghaza huko Palesitna.
-
Raisi: Kinachotokea katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu ni kielelezo cha jinai dhidi ya binadamu
Oct 12, 2023 08:38Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa: Kile kinachotokea katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu na Ukanda wa Ghaza dhidi ya raia wa Palestina ni kielelezo cha jinai dhidi ya binadamu.
-
Katika mazungumzo yao ya kwanza: Rais wa Iran na Mwanamfalme wa Saudia wajadili hali ya Gaza
Oct 12, 2023 05:55Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Mrithi wa Kiti cha Ufalme wa Saudi Arabia wamezungumza kwa njia ya simu kuhusu matukio ya Palestina na ulazima wa kusitishwa jinai za kivita zinazofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Gadi za pwani za Iran zafanya mazoezi makubwa ya kijeshi fukwe za kusini
Oct 11, 2023 09:15Gadi za Pwani za Iran zimeanza mazoezi makubwa ya kijeshi katika fukwe za Ghuba ya Uajemi, Bahari ya Oman na kaskazini ya Bahari Hindi.
-
Iran: Tuko tayari kuongoza mkutano wa nchi za Kiislamu kujadili Palestina
Oct 10, 2023 10:10Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu ipo tayari kuwa mwenyeji wa mkutano wa dharura wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC), kwa ajili ya kuzungumzia kadhia ya Palestina.
-
"Operesheni ya al-Aqsa imegeuza ndoto ya kuporomoka Israel kuwa uhalisia"
Oct 09, 2023 03:50Mkuu wa Komandi Kuu ya Vikosi vya Ulinzi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema ndoto na jinamizi la kuangamia na kupomoka kwa utawala wa Kizayuni wa Israel sasa imegeuka kuwa hali halisi kutokana na Operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa.
-
Kan'ani: Tuzo ya Amani ya Nobel inatolewa kisiasa
Oct 07, 2023 03:57Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amekosoa hatua ya waandaaji wa Tuzo ya Amani ya Nobel kumpa tuzo hiyo mwanamke wa Kiirani ambaye ameshitakiwa mara kadhaa kwa kufanya vitendo vya jinai hapa nchini.
-
Rais Ebrahim Raisi: Madola yanayowaunga mkono magaidi yanabeba dhima ya shambulizi la Damascus
Oct 06, 2023 23:53Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amelaani shambulio la kigaidi lililotokea Syria akisema waungaji mkono wa kigeni wa magaidi, wakiwemo wale wanaokalia kwa mabavu ardhi za nchi hiyo, ndio wanaobeba dhima ya hujuma hiyo.
-
Qalibaf aendelea na mashauriano huko Abu Dhabi; akutana na Rais wa Imarati
Oct 06, 2023 04:20Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge) amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) kuhusu kustawisha uhusiano wa pande mbili.