-
Amir-Abdollahian: Afrika ni moja ya vipaumbele vikuu vya diplomasia ya kiuchumi ya Iran
Aug 25, 2022 06:54Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran aliyeko ziarani nchini Tanzania amesema kuwa, bara la Afrika ni moja ya vipaumbele vikuu vya diplomasia ya kiuchumi ya Iran.
-
Iran kuunda ndege ya abiria ya viti 50 karibuni
Aug 24, 2022 23:11Mkuu wa Shirika la Uchukuzi wa Anga la Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu imeandaa mikakati ya kuzalisha ndege yake ya abiria karibuni hivi.
-
Iran: Israel inapaswa kuharibu silaha zake za nyuklia na ijiunge na NPT
Aug 23, 2022 23:50Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa ameutaka utawala wa Kizayuni wa Israel uharibu silaha zake za nyuklia na ujiunge haraka na Mkataba za Kuzuia Uzalishaji na Usambazaji wa Silaha za Nyuklia (NPT).
-
Jeshi la Iran kufanya maneva ya kijeshi ya droni
Aug 23, 2022 23:48Jeshi la Iran leo Jumatano linatazamiwa kuzindua luteka ya kijeshi itakayohusisha ndege zisizo na rubani (droni).
-
Jenerali Hajizadeh: Leo tunauza nje ya nchi makombora na ndege zisizo na rubani
Aug 23, 2022 03:31Kamanda wa Kikosi cha Anga za Mbali cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu IRGC amesema: "huko nyuma, sisi hatukuwa na wowote kati ya uwezo tulionao leo hii, na hivi sasa tunauza nje ya nchi makombora na ndege zisizo na rubani.
-
Rais Ebarahim Raisi: Iran ni tumaini la wanyonge na majuto kwa mabeberu
Aug 22, 2022 20:55Rais Ebrahim Raisi amesema kuwa, licha ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kuwa chini ya mashinikizo makubwa ya kila upande kwa makumi ya miaka sasa, lakini vijana wa nchi hii wakiwemo wa sekta ya ulinzi wamepiga hatua kubwa ya kujivunia.
-
Iran: Hatujapokea jibu la US kuhusu mapendekezo ya Ulaya
Aug 22, 2022 06:50Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu haijapokea majibu kutoka kwa Marekani juu ya mapendekezo yaliyotolewa na Umoja wa Ulaya kuhusu mapatano ya nyuklia ya JCPOA.
-
Salami: Hujuma dhidi ya nafsi na akili, stratejia hatari ya adui
Aug 21, 2022 23:53Kamanda Mkuu wa Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) ametahadharisha kuwa, stratejia hatari zaidi ambayo adui ameamua kutumia ni vita vya kinafasi na kisaikolojia.
-
Ibrahim Raeisi: Hakuna mazungumzo yoyote yatakayoifanya Iran ilegeze msimamo katika haki zake
Aug 21, 2022 06:47Rais Ibrahim Raeisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, hakuna kikao au mazungumzo yoyote yale ambayo yatalifanya taifa hili lilegeze kamba na kufumbia macho haki zake.
-
Wazayuni wajuta kumshinikiza Trump ajitoe katika makubaliano ya nyuklia JCPOA mwaka 2018
Aug 20, 2022 22:15Wakuu wa masuala ya usalama wa utawala haramu wa Kizayuni wa Israel wameonyesha majuto kwa hatua ya utawala huo ya kumshinikiza rais wa zamani wa Marekani Donald Trump ajitoe kwenye makubaliano ya nyuklia JCPOA mwaka 2018.