-
Tofauti kati ya safari ya Biden na Putin eneo la Asia Magharibi
Jul 19, 2022 04:04Baada ya safari ya Rais Joe Biden wa Marekani katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu (Israel) na Saudi Arabia, Rais Vladimir Putin wa Russia leo yuko safarini nchini Iran. Kuna tofauti za wazi kati ya malengo na ajenda za safari ya Biden na Putin katika eneo la Asia Magharibi. Rais Tayyip Erdoğan wa Uturuki pia yuko safarani nchini Iran kwa lengo la mkutano wa pande tatu wa marais wa Iran, Russia na Uturuki.
-
Iran yaipongeza Iraq kwa kushajiisha mazungumzo katika eneo
Jul 18, 2022 03:32Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ameipongeza Iraq kwa nafasi yake athirifu na jitihada zake za kushajiisha utumiaji wa mazungumzo kwa ajili ya kujaribu kutatua matatizo na changamoto zinaolikabili eneo hili la Asia Magharibi.
-
Iran yawawekea vikwazo Wamarekani wanaounga mkono magaidi wa MKO
Jul 16, 2022 23:05Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imetangaza orodha mpya ya maafisa wa sasa na wa zamani wa serikali ya Marekani ambao kwa makusudi wamekuwa wakiunga mkono kundi la kigaidi la MKO lililo dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Jen. Shekarchi: Marekani, Israel zinajua vyema gharama ya kuitishia Iran
Jul 15, 2022 22:14Msemaji wa Vikosi vya Ulinzi vya Iran amesema Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel zinatambua vizuri kile ambacho kitawafika iwapo zitathubutu kutelekeza kivitendo vitisho vyao dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu.
-
Shukurani za Gavana wa jimbo la Herat kwa misaada ya Iran kwa watu wa Afghanistan
Jul 15, 2022 22:12Gavana wa jimbo la Herat ameishukuru Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa misaada yake kwa watu wa Afghanistan.
-
Kamanda: Vikosi vya Jeshi la Iran vinaendelea kuimarika licha ya vikwazo
Jul 14, 2022 21:58Kamanda Mkuu wa Kikosi cha Anga cha Jeshi la Nchi Kavu la Iran amesema vikosi vya ulinzi vya Jamhuri ya Kiislamu vinendelea kuimarika na kupata nguvu zaidi siku baada ya siku, licha ya vikwazo na mashinikizo ya kiuchumi dhidi ya taifa hili.
-
Kan’ani Chafi: Hadaa ni sifa iliyoshamiri ya wanasiasa wa Marekani
Jul 14, 2022 06:01Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema hadaa na kusema uongo ni sifa ya kawaida katika kauli za wanasiasa wa Marekani.
-
Iran: Israel ndio mzizi wa ugaidi na ukosefu wa usalama Asia Magharibi
Jul 12, 2022 22:58Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema utawala wa Kizayuni wa Israel ndio chimbuko la vitendo vya kigaidi na ukosefu wa usalama na uthabiti katika eneo hili la Asia Magharibi.
-
Iran yapinga mpango wa US kuunda mfumo wa ulinzi katika eneo
Jul 11, 2022 06:59Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imeutaja mpango wa Marekani wa kutaka kuunda eti mfumo wa pamoja wa ngao ya makombora katika eneo hili kuwa ni wa kichochezi na kichokozi.
-
Iran kati ya nchi 15 zinazovutia idadi kubwa ya wanafunzi wa kigeni
Jul 11, 2022 06:31Iran imetajwa kuwa miongoni mwa nchi 15 duniani, zenye kuvutia idadi kubwa ya wanafunzi wa kigeni.