-
Mkutano wa siri wa wakuu wa Israel na UAE kupanga njama dhidi ya Iran wafichuka
Aug 16, 2019 02:58Maafisa wa ngazi za juu wa utawala haramu wa Israel na Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) hivi karibuni walifanya mkutano wa siri kwa lengo la kupanga njama dhidi ya Iran.
-
Zarif: Meli ya mafuta ya Iran ilikuwa imezuiwa kinyume cha sheria
Aug 15, 2019 22:46Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amekanusha madai ya serikali ya Uingereza kuwa meli ya mafuta ya Iran ya Grace 1 ilikuwa imekiuka sheria za Umoja wa Ulaya kuhusu vikwazo.
-
Sisistizo la anayechukua nafasi ya Mogherini na Troika ya Ulaya kuhusu kulinda JCPOA
Aug 15, 2019 05:44Umoja wa Ulaya na Troika ya umoja huo yaani, Ujerumani, Ufaransa na Uingereza, kama wanachama wa kundi la 4+1 wamekuwa wakidai kuwa wanaunga mkono mapatano ya nyuklia ya Iran maarufu kama JCPOA. Pamoja na hayo, hivi sasa Ulaya inakabiliwa na changamoto kubwa katika kulinda mapatano ya JCPOA. Ni kwa msingi huo ndio wakuu wa Umoja wa Ulaya na Troika ya Ulaya wakasisitiza kuhusu kulinda JCPOA.
-
Uungaji mkono wa Shekhe wa Muqawama kwa diplomasia ya Zarif
Aug 15, 2019 03:26Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon amemtumia ujumbe Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, ambapo sambamba na kulaani hatua ya Marekani ya kumwekea vikwazo Mohammad Javad Zarif amesisitizia mshikamano wa muqawama kwa mwanadiplomasia huyo.
-
Iran: Uingereza inatarajiwa baada ya muda si mrefu kuiachia meli ya mafuta iliyoizuia
Aug 13, 2019 22:06Shirika la Bandari na Safari za Majini la Iran limesema, Uingereza inatazamiwa baada ya muda si mrefu kuiachia meli ya mafuta inayomilikiwa na Iran ambayo iliizuia kinyume cha sheria mwezi uliopita katika pwani ya Gibraltar, baada ya pande mbili kubadilishana baadhi ya nyaraka ili kurahisisha kuachiwa kwa meli hiyo.
-
Uchochezi wa mitandao ya kijamii katika nchi zinazopinga sera za Marekani
Aug 13, 2019 03:42Katika kipindi chote cha utawala wa Rais Vladmir Putin nchini Russia Wamagharibi wamekuwa wakifanya kila wawezalo kuzusha ghasia na kuingilia masuala ya ndani ya nchi hiyo. Nchi za Magharibi hususan Marekani, zimekuwa zikitumia zaidi propaganda chafu na vita vya kinafsi dhidi ya Russia na nchi nyingine zisizokubaliana na sera zao za kibeberu.
-
Jahangiri: Marekani inalenga kuvuruga usalama wa Ghuba ya Uajemi
Aug 13, 2019 02:43Makamu wa Kwanza wa Rais wa Iran Eshaq Jahangiri amesema Marekani inalenga kuvuruga usalama wa Ghuba ya Uajemi na Lango Bahari la kistratijia la Hormuz na kutumia ukosefu wa usalama kama kisingizo cha kujiimarisha kijeshi katika eneo.
-
Pakistan yaiomba Iran isaidie utatuzi wa amani wa mgogoro wa Kashmir
Aug 11, 2019 02:16Pakistan imetoa wito kwa jamii ya kimataifa, ikiwemo Iran, kusaidia katika kutafutia suluhisho la amani mgogoro wa Kashmir baada ya kuibuka uhasama mpya baina ya India na Pakistan kuhusu eneo hilo linalozozaniwa.
-
Usalama wa Ghuba ya Uajemi utadhaminiwa kwa ushirikiano wa majirani
Aug 09, 2019 04:59Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amejadiliana, kupitia mazungumzo ya simu, na Mawaziri wenzake wa Ulinzi wa Qatar, Oman na Kuwait kuhusu umuhimu wa kudhaminiwa usalama wa Ghuba ya Uajemi kupitia ushirikiano wa pamoja.
-
Saudi Arabia na Bahrain, "makuwadi wa kisiasa" wa Marekani
Aug 09, 2019 03:43Marekani imekuwa ikiitisha vikao na mikutano kwa shabaha ya kutangaza sera zake za kueneza propaganda chafu dhidi ya Iran na sasa vikao hivyo vinafanyika katika nchi ndogo ya Bahrain.