-
Zarif: Sidhani vita baina ya Iran na Marekani vinakaribia, lakini...
May 03, 2019 03:23Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Mohammad Javad Zarif amesema hadhani vita baina ya Iran na Marekani vinakaribia lakini ametahadharisha kuwa, kuna 'ajali zinazoweza kutokea' na kubadilika kuwa makabiliano ya kijeshi.
-
Iran yalaani jaribio la Marekani la kutaka kuipindua serikali ya Venezuela
May 02, 2019 23:27Iran imelaani jaribio la hivi karibuni la Marekani la kutaka kuipindua serikali halali ya Rais Nicolas Maduro wa Venezuela.
-
OPEC: Ni muhali kuyaondoa mafuta ya Iran katika soko la dunia
May 02, 2019 09:10Katibu Mkuu wa Shirika la Nchi Zinazouza Mafuta kwa Wingi Duniani (OPEC) amesema ni muhali kuyaondoa mafuta ya Iran katika soko la kimataifa na kwamba shirika hilo linafanya juu chini kuhakikisha kuwa siasa haziingizwi katika biashara ya mafuta.
-
Kusimamishwa uuzaji wa mafuta ya Iran, ni ukweli au ndoto?
May 02, 2019 07:30Waziri wa Mafuta wa Iran amesema, hata kama kukatwa kabisa na kufikishwa katika kiwango cha sufuri uuzaji nje wa mafuta ya Iran ni matarjio ya Marekani na nchi mbili jirani na Iran, lakini jambo hilo halitekelezeki kivitendo.
-
Kama si Iran leo Iraq na Syria zingekuwa zimegawanyika vipande vipande
May 02, 2019 03:29Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran asema uthabiti na usalama katika eneo umepatikana kwa gharama kubwa na kuongeza kuwa: "Kama si ushirikiano wa kujitolea wa Iran, leo Iraq na Syria zingekuwa zimegawanyika vipande vipande mikononi mwa waovu na maadui wa amani na usalama."
-
Kamati ya Nyuklia ya Iran: Tutajiondoa NPT, JCPOA iwapo tutaendelea kuwekewa vikwazo
May 01, 2019 03:07Mwenyekiti wa Kamati ya Nyuklia ya Majilisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amesema iwapo taifa hili litaendelea kukabiliwa na vikwazo, basi Tehran itajitoa katika Mkataba wa Kuzuia Uzalishaji na Uenezaji wa Silaha za Atomiki (NPT) sambamba na makubaliano ya nyuklia ya JCPOA.
-
Rais Rouhani asaini sheria ya kuitambua CENTCOM ya Marekani kuwa kundi la kigaidi
Apr 30, 2019 22:41Rais Hassan Rouhani wa Iran amesaini kuwa sheria, muswada wa kuwatambua wanajeshi wote wa Marekani katika eneo la Asia Magharibi (CENTCOM) na vikosi vyote vinavyofungamana nao kuwa kundi la kigaidi.
-
Pompeo atoa vitisho dhidi ya wanunuzi wa mafuta ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran
Apr 30, 2019 02:47Kufuatia radiamali hasi ya kimataifa kuhusiana na vikwazo vipya vya mafuta vya Marekani dhidi ya Iran, Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo kwa mara nyingine tena amewatishia wanunuzi wa mafuta ya nchi hii.
-
IMF: Vikwazo vya Marekani dhidi ya Iran vinavuruga ukuaji wa uchumi katika eneo
Apr 29, 2019 02:24Mfuko wa Fedha Duniani (IMF) umesema vikwazo vya Marekani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran vimedumaza ukuaji wa uchumi katika eneo la Asia Magharibi.
-
Marekani ni hatari kubwa kwa mustakbali wa dunia
Apr 29, 2019 02:01Mwanafikra wa Kiislamu kutoka visiwa vya Komoro amesema kuwa Marekai imehatarisha usalama wa dunia kutokana na siasa zake mbovu za kuingilia mara kwa mara mambo ya ndani ya nchi nyingine.