-
Rais Pezeshkian: Hakuna nchi inayoweza kuipigisha magoti Iran yenye umoja
Jul 31, 2025 09:06Rais Masoud Pezeshkian wa Iran amesema kuwa hakuna nchi inayoweza kuwapigisha magoti wananchi wa Iran na hakuna kizuizi chochote kinachoweza kukwamisha ustawi wao madhali wanadumisha umoja na mshikamano wao.
-
Malengo halisi ya Magharibi kuhusu Iran ni yapi?
Jul 30, 2025 08:29Vyombo vya habari vya kigeni, sambamba na kuripoti kauli ya hivi karibuni ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, vimezingatia kwa namna ya kipekee sehemu ya hotuba yake ambapo amesisitiza kuwa: “Mpango wa nyuklia, urutubishaji na haki za binadamu ni visingizio – wanachotaka wao ni dini na elimu yenu.”
-
Qalibaf: Mauaji ya kimfumo ya Wapalestina huko Gaza yanakumbusha jinai za Wanazi
Jul 30, 2025 04:10Mohammad Baqer Qalibaf Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge) amelaani mauaji ya kimfumo ya Wapaletsina yanayotekelezwa na utawala wa Israel katika Ukanda wa Gaza na kuyataja kuwa yanakumbusha jinai zilizofanywa na Wanazi wakati wa Vita vya Pili vya Dunia.
-
Kwa nini Marekani imeitaka China iache kununua mafuta ya Iran?
Jul 27, 2025 23:03Waziri wa Fedha wa Marekani ametoa wito kwa China kuacha kununua mafuta ya Iran na Russia wakati huu inapokaribia duru mpya ya mazungumzo ya ushuru wa forodha kati ya Marekani na China.
-
Matokeo ya Mkutano wa Istanbul kati ya Iran na Troika ya Ulaya
Jul 26, 2025 09:10Suala la kuondoa vikwazo na kutilia mkazo haki ya Iran ya kurutubisha urani ni miongoni mwa mambo yaliyojadiliwa katika ajenda ya "Mkutano wa Istanbul." Pande hizo zimesisitiza udharura wa kuendeleza mazungumzo.
-
Wanafunzi wa Iran washinda medali tano katika Mashindano ya Kimataifa ya Fizikia 2025
Jul 25, 2025 23:01Timu ya wanafunzi wa shule za upili kutoka Iran imejinyakulia medali tano za fedha katika Mashindano ya 55 ya Kimataifa ya Fizikia (International Physics Olympiad - IPhO 2025) yaliyofanyika jijini Paris, Ufaransa.
-
Helikopta ya Jeshi la Wanamaji la Iran yaitimua manowari ya US katika Bahari ya Oman
Jul 24, 2025 03:25Helikopta ya Jeshi la Wanamaji la Iran imeitimua manowari ya mashambulizi ya Marekani iitwayo USS Fitzgerald katika Bahari ya Oman, kwa kutoa ishara za onyo na hatimaye kuilazimisha ibadili mkondo wake kuelekea upande wa kusini wa eneo hilo.
-
Iran yaalani ukatili mkubwa wa sera ya njaa na mauaji ya Israel dhidi ya wakazi wa Gaza
Jul 23, 2025 07:37Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imelaani " ukatili mkubwa" unaofanywa na utawala ghasibu wa Israel, na kulaani sera ya njaa na mauaji ya utawala huo dhidi ya Wapalestina wanaotafuta misaada huko Gaza.
-
Rais Pezeshkian: Ziitwazo ‘haki za binadamu’ na ‘asasi za kimataifa’ si chochote ila ni uwongo tu
Jul 22, 2025 10:25Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, zinazoitwa haki za binadamu na asasi za kimataifa si chochote zaidi ya uwongo tu na akabainisha kwamba, katika dunia ya leo iliyostaarabika na mbele ya macho ya watu wote, wanawakatia maji na chakula watu wanyonge, wanawake na watoto na kufanya mauaji ya kimbari; kisha wanazungumzia haki za binadamu, huku wao wenyewe wakiwa wamekiuka vipimo vyote vya kimataifa na haki za binadamu na kufanya jinai dhidi ya ubinadamu kila mahali dunian
-
Iran, Uturuki: Ulimwengu wa Kiislamu uchukue hatua dhidi ya mauaji ya kimbari yanayofanywa na Israel Ghaza
Jul 22, 2025 07:36Mawaziri wa mambo ya nje wa Iran na Uturuki wametoa wito kwa mataifa ya Kiislamu duniani kuchukua hatua kali za kusaidia kukomesha vita vya miezi 21 vya mauaji ya kimbari vinavyoendelezwa na utawala wa kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Ghaza.