-
Meja Jenerali Salami: Wazayuni wakifanya kosa, jibu letu litakuwa la kuumiza sana
Oct 17, 2024 08:14Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran (SEPAH) amesema kuwa, utawala wa Kizayuni wa Israel na viongozi wake wanapaswa kutambua kuwa, Operesheni ya Ahadi ya Kweli-2 lilikuwa onyo tu na kama Israel itakosea na kuthubutu kufanya uvamizi, jibu la Iran litakuwa la kuumiza sana.
-
Waziri wa Ulinzi wa Iran: Mfumo wa ulinzi wa Marekani wa THAAD si jambo jipya
Oct 16, 2024 23:25Waziri wa Ulinzi wa Iran ameeleza kuwa mfumo wa ulinzi wa Marekani wa THAAD si jambo jipya na kwamba Iran unalichukulia suala hilo kuwa ni sehemu ya vita vya kisaikolojia na sio tatizo mahsusi.
-
Iran yazitaka nchi za Shanghai kuwa jadi dhidi ya jinai za Israel na ugaidi wa kiuchumi wa Marekani
Oct 16, 2024 23:24Mkuu wa ujumbe wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Mkutano wa Jumuiya ya ushirikiano ya Shanghai (SCO) huko Pakistan ameitaka jumuiya hiyo kuwa jadi na kuchukua hatua madhubuti dhidi ya chokochoko za utawala wa Kizayuni na ugaidi wa kiuchumi wa Marekani. Amezitaka nchi wanachama wa Shanghai kuchukua hatua za kivitendo ili kukabiliana na vikwazo vya kibiashara vya pande zote.
-
Sisitizo la Joe Biden la kudumisha uwepo wa kijeshi wa Marekani Asia Magharibi
Oct 16, 2024 10:00White House ilitangaza siku ya Jumanne kwamba, Rais Joe Biden wa Marekani ameiandikia barua Congress ya nchi hiyo akiifahamisha kwamba vikosi vya Marekani vitaendelea kubakia katika eneo la Asia Magharibi (Mashariki ya Kati) kwa kuhofia jibu la Iran kwa chokochoko za utawala wa Kizayuni.
-
Ghalibaf: Ulimwengu wa Kiislamu unapaswa kusitisha ushirikiano wa kisiasa na kiuchumi na utawala wa Kizayuni
Oct 13, 2024 22:53Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema: Tunahitaji kukkomesha aina yoyote ya ushirikiano, msaada na mazungumzo na utawala wa Kizayuni wa Israel na kusimamisha aina yoyote ya mpango wa kisiasa na kiuchumi unaousaidia utawala huo.
-
Araqchi akanusha Iran kuipatia Russia makombora ya balistiki
Oct 13, 2024 09:28Iran kwa mara nyingine tena imekadhibisha madai kuhusu kuipatia Russia makombora ya balistiki kufuatia ripoti kwamba Umoja wa Ulaya utatumia tuhuma hizo kama kisingizio cha kuwekea vikwazo Jamhuri ya Kiislamu.
-
Iran yakanusha madai ya kuhusika na operesheni ya Wapalestina ya Kimbunga cha Al Aqsa
Oct 13, 2024 03:40Ujumbe wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa umepuuzilia mbali ripoti za vyombo vya habari vya Marekani zinazodai kuwa Jamhuri ya Kiislamu ilikuwa na taarifa kuhusu Operesheni ya Kimbunga cha al-Aqsa iliyotekelezwa mwaka jana na wapigania ukombozi wa Palestina dhidi ya utawala wa Israel.
-
Iran: Tutatoa jibu madhubuti kwa nchi zitakazokubali kutumiwa kutushambulia
Oct 12, 2024 23:14Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amesema Jamhuri ya Kiislamu itajibu mapigo dhidi ya nchi ambazo zitaruhusu anga na ardhi zao zitumiwe kulishambulia taifa hili.
-
Iran: Walimwengu wachukue hatua kukabiliana na jinai za utawala wa Kizayuni
Oct 12, 2024 03:52Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran amesema kuwa, walimwengu wanapaswa kuchukua hatua za pamoja kukabiliana na hatua za kishari na jinai za utawala haramu wa Israel.
-
Rais wa Iran asisitizia umuhimu wa umoja wa Waislamu
Oct 11, 2024 07:48Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian amesisitiza haja ya umma wa Kiislamu kuwa na umoja na mshikamano na kubainisha kwamba, migawanyiko kati ya Waislamu itawanufaisha maadui pekee.