-
Kiongozi Muadhamu: Watu wa Iraq, Lebanon wafuatilie matakwa yao ya haki kwa njia za kisheria
Oct 30, 2019 08:32Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameashiria njama za maadui za kuvuruga usalama katika baadhi ya nchi za eneo na kusema: "Wanaojali Iraq na Lebanon wafahamu kuwa, kipaumbele chao kinapaswa kuwa kuondoa hali ya ukosefu wa usalama na wananchi wa nchi hizo nao wafahamu kuwa, matakwa yao ya haki yanaweza tu kukidhiwa katika fremu ya mfumo wa kisheria."
-
Mousavi: Iraq na Syria ziliisambaratisha kitambo ISIS kwa msaada wa Iran
Oct 28, 2019 08:51Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh (ISIS) lilisambaratishwa na Iraq na Syria muda mrefu umepita, kwa msaada wa kilojistiki wa Jamhuri ya Kiislamu.
-
Muosavi: Iran inafuatilia kwa makini matukio ya Iraq
Oct 27, 2019 04:02Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ameeleza kusikitishwa kwake na yanayojiri katika nchi jirani ya Iraq ambayo yamepelekea kuuawa na kujeruhiwa makumi ya watu na kuharibiwa mali ya umma na kusema: Tehran inafuatilia kwa makini yanayojiri nchini humo.
-
Iraq yasema maafisa wa usalama hawajatumia silaha dhidi ya waandamanaji
Oct 26, 2019 23:08Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Iraq amesema vikosi vya usalama nchini humo havijatumia silaha dhidi ya waandamanaji katika maandamano ya hivi karibuni nchini humo.
-
Ayatullah Sistani atahadharisha juu ya ghasia na kuandaliwa mazingira ya uingiliaji wa kigeni nchini Iraq
Oct 25, 2019 23:05Mwakilishi wa marjaa mkubwa nchini Iraq ametahadharisha kuhusiana na kutoka maandamano katika mkondo wa amani na kuibuka ghasia ambazo zitaandaa mazingira ya uingiliaji wa madola ya kigeni nchini humo.
-
Mauaji ya kigaidi yaongezeka Iraq baada ya Marekani kuwahamishia nchini humo magaidi wa ISIS
Oct 25, 2019 03:42Mauaji ya kigaidi yameongezeka dhidi ya maafisa wa serikali ya Iraq baada ya Marekani kuwahamishia nchini humo magaidi wa Daesh (ISIS) kutoka kaskazini mwa Syria kufuatia kushadidi mashambulizi ya Uturuki huko Syria.
-
Matukio yanayojiri Iraq; harakati inayofuata njia tata zaidi na muelekeo usiotabirika
Oct 24, 2019 23:02Matukio yanayojiri nchini Iraq yanaelekea kwenye njia tata zaidi na muelekeo usiotabirika, kufuatia safari ya Waziri wa Ulinzi wa Marekani nchini humo na msimamo wa wapinzani wa serikali wa kufanya maandamano Ijumaa ya leo ya tarehe 25 Oktoba.
-
Jeshi la Iraq: Askari wa Marekani hawana haki ya kuwepo ndani ya nchi hii
Oct 22, 2019 08:16Kamandi ya jeshi la Iraq sambamba na kutoa taarifa imesema kuwa, askari wa Marekani ambao wametokea Syria, wanaweza tu kuitumia Iraq kama njia ya kuvuka na kwamba hawana haki ya kuweka kambi nchini humo.
-
Zaidi ya wafanyaziara milioni 17 wameshiriki katika Arubaini ya Imam Hussein (as) ya mwaka huu
Oct 20, 2019 23:09Gavana wa mkoa wa Karbala nchini Iraq ametangaza kuwa, idadi ya mazuwari walioshiriki kwenye maombolezo ya Arubaini ya Imam Hussein (as) mwaka huu imepindukia milioni 17.
-
Mamia ya askari wa Marekani wanaoondolewa Syria kupelekwa Iraq
Oct 20, 2019 04:00Waziri wa Ulinzi wa Marekani amesema mamia ya wanajeshi wa nchi hiyo wanaoondolewa Syria watapelekwa nchini Iraq.