Feb 05, 2021 07:19
Shughuli za kibiashara zimerejea tena katika mji wa Bangassou, nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR baada ya askari wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa wa ujumbe wa umoja huo nchini humo, MINUSCA kuimarisha doria ili kudhibiti vitisho vyovyote kutoka kwa waasi waliosababisha maelfu ya watu kukimbia makwao kufuatia mashambulizi ya mwezi uliopita wa Januari.