-
Zarif: Marekani ikichukua uamuzi usio sahihi kuhusu JCPOA, itakabiliwa na jibu mwafaka la Iran
May 07, 2018 03:31Waziri wa Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, endapo Marekani itakosea na kuchukua uamuzi usio sahihi kuhusiana na makubaliano ya nyuklia yanayojulikana kama Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji (JCPOA), itakkabiliwa na jibu linalofaa kutoka kwa Iran.
-
Velayati: Iran itachukua hatua inayofaa endapo Marekani itajiondoa katika makubaliano ya JCPOA
May 06, 2018 22:28Mshauri wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu katika masuala ya kimataifa amesema kuwa, endapo Marekani itajiondoa katika makubaliano ya nyuklia ya JCPOA, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran itatoa jibu mwafaka kulingana na mazingira yalivyo.
-
Rais Rouhani: JCPOA ni dhihirisho la nguvu za kidiplomasia za taifa kubwa la Iran
May 06, 2018 12:25Rais Hassan Rouhani amesema: Makubaliano ya nyuklia ya JCPOA ambao ni mkataba wa kimataifa na dhihirisho la nguvu za kidiplomasia za taifa kubwa la Iran hauwezi kufanyiwa mabadiliko yoyote.
-
Hatua zenye kukinzana za Uingereza kuhusu makubaliano ya JCPOA
May 06, 2018 03:16Ikiwa imekaribia muda wa kuchukuliwa uamuzi na Rais wa Marekani kuhusu makubaliano ya nyuklia yaliyofikiwa kati ya kundi la 5+1 na Iran, juhudi za kimataifa pia zimeongezeka ili kuishaiwishi nchi hiyo itekeleze ahadi na majukumu yake kimataifa.
-
Shamkhani: JCPOA ni mtihani wa kihistoria kwa ufanisi wa taasisi za kimataifa
May 05, 2018 22:06Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran amesema kudumu au kuvunjika makubaliano ya nyuklia ya JCPOA, yakiwa ni makubaliano ya kisiasa na kiusalama yaliyothibitishwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ni mtihani wa kihistoria wa kutathmini taathira ya mantiki ya mazungumzo badala ya mizozo na vilevile kiwango cha ufanisi wa taasisi za kimataifa.
-
Indhari ya Russia kuhusu kufutwa makubaliano ya JCPOA na taathira zake mbaya
May 05, 2018 07:39Serikali ya Russia imetoa taarifa ikisisitiza kuwa makubaliano ya nyuklia ya JCPOA ni utaratibu ulio na mlingano weenye manufaa ya pande zote na kutahadharisha kuwa kuvunjwa makubaliano hayo kutakuwa kwa madhara. Kwa mujibu wa taarifa hiyo ya Russia, kuvurugwa mlingano unaolegalega wa kimaslahi ndani ya makubaliano ya JCPOA kutakuwa na taathira kuu kwa usalama wa kimataifa na muundo unaopiga marufuku uenezaji wa silaha za nyuklia.
-
Ufaransa: Kuihifadhi JCPOA ni kipaumbele chetu, kujitoa ni kutangaza vita
May 05, 2018 03:23Mwakilishi wa kudumu wa Ufaransa katika Umoja wa Mataifa amesema kuwa, kuyalinda mapatano ya nyuklia ya Iran maarufu kwa jina la JCPOA ndicho kipaumbele cha nchi yake.
-
Russia: Iwapo Marekani itajitoa katika JCPOA, itabidi iwekewe vikwazo
May 05, 2018 03:22Afisa mmoja wa Russia amesisitiza kuwa, kama Marekani itajitoa katika mapatano ya nyuklia ya JCPOA, itabidi iwekewe vikwazo vya kimataifa.
-
Ujumbe Muhimu wa Zarif kuhusu mapatano ya nyuklia ya Iran + VIDEO
May 04, 2018 12:03Katika Ujumbe wake wa video hapo jana Alkhamisi, Muhammad Jawad Zarif, Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran alisema kuwa kuna chaguo moja tu la kufanikisha makubaliano ya nyuklia kati ya Iran na nchi sita kubwa za dunia, nalo ni Marekani kutekeleza ahadi zake zote kuhusiana na makubaliano hayo.
-
Ujumbe wa Zarif: Mapatano ya JCPOA ima yatabakia katika mfumo wake wa sasa au yavunjike kabisa
May 04, 2018 08:08Katika Ujumbe wake wa video hapo jana Alkhamisi, Muhammad Jawad Zarif, Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran alisema kuwa kuna chaguo moja tu la kufanikisha makubaliano ya nyuklia kati ya Iran na nchi sita kubwa za dunia, nalo ni Marekani kutekeleza ahadi zake zote kuhusiana na makubaliano hayo.