-
Katibu Mkuu wa UN: JCPOA ni ushindi muhimu wa kidiplomasia
May 04, 2018 02:55Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ameonya dhidi ya kuvunjwa makubaliano ya nyuklia ya Iran huku akisisitiza kuwa mapatano hayo ni ushindi muhimu wa kidiplomasia ambayo yanapaswa kulindwa.
-
Malengo mawili ya makelele mapya ya Netanyahu dhidi ya Iran
May 04, 2018 02:20Benjamin Netanyahu, Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni, Jumatatu usiku aliendeleza vitendo vyake vya chuki na ghilba za kisiasa dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa kuonesha mbele ya kamera za vyombo vya habari vitu alivyodai kuwa eti ni ushahidi kwamba Iran inafanya juhudi za siri za kumiliki silaha za nyuklia.
-
Zarif: Iran haitofanya mazungumzo yoyote kuhusu JCPOA na mapatano hayo hayataongezwa chochote
May 03, 2018 23:42Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema katika ujumbe alioutoa jana kwa njia ya video kwamba Tehran haitofanya mazungumzo yoyote mapya kuhusu JCPOA na wala mapatano hayo ya nyuklia hayataongezwa chochote. Amesema mapatano hayo yana njia moja tu nayo ni Marekani kuheshimu vipengee vyake vyote.
-
Najafi: Matumizi ya nishati ya nyuklia kwa malengo ya kiraia ni haki ya nchi zote
May 03, 2018 02:20Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Nyuklia (IAEA) amesisitiza kuwa nchi ambazo zinamiliki mabomu ya nyuklia hazina haki ya kuzuia nchi nyingine zistafidi na teknolojia ya nyuklia kwa malengo ya amani kwa kisingizio cha kuzuia kuenezwa silaha hizo.
-
China: Pande zote zinapaswa kuheshimu mapatano ya JCPOA
May 02, 2018 21:17China imesisitizia umuhimu wa pande zote husika kuendelea kufungamana na mapatano ya nyuklia ya Iran yanayojulikana kwa kifupi kama JCPOA.
-
Boroujerdi: Kama vikwazo dhidi ya Iran vitarejeshwa hakutakuwa na haja ya kuendelea na JCPOA
May 02, 2018 21:17Mkuu wa Kamati ya Usalama wa Taifa na Siasa za Kigeni ya Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amesema kuwa, kama vikwazo vitarejeshwa, hakutakuwa na kitu chochote cha kuweza kuwakinaisha wananchi, Serikali na Bunge la Iran na kuwafanya wakubali kuendelea kuwemo katika mapatano ya nyuklia ya JCPOA.
-
Waziri Mkuu wa zamani wa Israel: Madai ya Netanyahu kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran hayana thamani yoyote
May 02, 2018 03:21Waziri Mkuu wa zamani wa Israel Ehud Barak amesema: matamshi ya Benjamin Netanyahu dhidi ya mpango wa nyuklia wa Iran hayana thamani yoyote.
-
Iran yaitaka Israel na waungaji mkono wake waache chokochoko zao la sivyo watajuta
May 01, 2018 23:17Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameuonya utawala haramu wa Israel na waungaji mkono wake na kuwataka waache njama na miamala yao hatari kwani jibu la Iran litakuwa la kushtukiza na la kuwafanya wajute.
-
Kupuuza Mogherini na Putin mchezo wa kitoto wa Benjamin Netanyahu
May 01, 2018 07:37Ikulu ya Russia Kremlin imetangaza kuwa, Rais Vladimir Putin wa nchi hiyo amefanya mazungumzo kwa njia ya simu na Benjamin Netanyahuu, Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel kuhusiana na makubaliano ya nyuklia ya JCPOA.
-
Mogherini ajibu mchezo wa kitoto wa Netanyahu kuhusu mapatano ya JCPOA
May 01, 2018 00:06Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya, usiku wa kuamkia leo amejibu mchezo wa kitoto wa Benjamin Netanyahu, waziri mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel aliyedai kuwa eti Iran haijaheshimu mapatano ya nyuklia ya JCPOA.