-
Haaretz: Iran; ajenda kuu ya mazungumzo ya Waziri mpya wa Mashauri ya Kigeni wa Marekani na Netanyahu
Apr 29, 2018 03:19Gazeti la Kizayuni la Haaretz limeripoti kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ni ajenda kuu itakayojadiliwa katika mazungumzo kati ya Mike Pompeo Waziri mpya wa Mashauri ya Kigeni wa Marekani na Benjamin Netanyahu Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni.
-
Iran: Tutasimama kidete kukabiliana na vikwazo vyovyote vile
Apr 28, 2018 23:07Msemaji wa serikali ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, hakuna kikwazo chochote kitakacholenga manufaa ya Jamhuri ya Kiislamu kitakachoachwa vivi hivi hivi bila ya kutumia uwezo wetu wote kupambana nacho.
-
Kutengwa Marekani katika Muungano wa (NATO) juu ya kadhia ya JCPOA
Apr 28, 2018 03:24Katibu Mkuu wa Muungano wa Kijeshi wa Nchi za Magharibi (NATO), Jens Stoltenberg ametoa matamshi yanayokinzana na mtazamo wa Rais Donald Trump wa Marekani kuhusiana na makubaliano ya nyuklia kati ya Iran na nchi sita kubwa za dunia yanayojulikana kama Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji JCPOA.
-
Sayyid Aboutorabi: Kwa miongo yote minne taifa la Iran limepambana vikali na udhalimu
Apr 27, 2018 09:20Mohammad-Hassan Aboutorabi Fard, khatibu wa swala ya Ijumaa iliyoswaliwa leo mjini Tehran amezungumzia njama za Rais Donald Trump wa Marekani kwa ajili ya kuharibu makubaliano ya nyuklia (JCPOA) na kusema, kwa miongo minne taifa la Iran limepambana na hatua za kiuhasama na kidhalimu zikiwemo za Marekani.
-
Russia yapinga matamshi ya Trump, Macron kuhusu makubaliano ya JCPOA
Apr 26, 2018 23:14Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia amepinga matamshi yaliyotolewa na Marais wa Marekani na Ufaransa kuhusu suala la kufanyiwa mabadiliko makubaliano ya nyuklia ya JCPOA.
-
Azma ya kimataifa kwa ajili ya kulinda mapatano ya JCPOA
Apr 26, 2018 08:41Huku tarehe 12 Mei ikiwa inakaribia, ambayo ni tarehe ya mwisho iliyoainishwa na Rais Donald Trump wa Marekani kwa ajili ya kufanyiwa marekebisho makubaliano ya nyuklia kati ya Iran na nchi sita kubwa za dunia yanayojulikana kama Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji JCPOA, radiamali na harakati za serikali na viongozi wa kundi la 5+1 kwa ajili ya kulinda mapatano hayo zimeongezeka.
-
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ataka mapatano ya nyuklia ya Iran yalindwe
Apr 26, 2018 03:24Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema mapatano ya nyuklia ya Iran yanayojulikana kama Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezwaji (JCPOA) yanapaswa kulindwa.
-
Zarif: Iran itafuata nyayo iwapo US itajiondoa kwenye makubaliano ya nyuklia
Apr 25, 2018 03:04Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Iran amesema kuna uwezekano mkubwa Iran itajiondoa kwenye makubaliano ya nyuklia ya JCPOA, iwapo Marekani itaamua kujivua kwenye mapatano hayo ya kimataifa ya mwaka 2015.
-
Shamkhani: Marekani na Ulaya zikivuka mstari mwekundu wa Iran zitagonga mwamba
Apr 24, 2018 22:02Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa nchini Iran amesema kuwa, iwapo Ulaya itafanya makosa ya kistratijia na kusalimu amri mbele ya Marekani na kuvuka mistari mnyekundu ya Iran kwa shabaha ya kutaka kumridhisha Donald Trump, hapana shaka kuwa itakula mweleka na kushindwa.
-
Rais Rouhani aonya kuhusu taathira hasi iwapo JCPOA itakiukwa
Apr 24, 2018 12:04Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameionya Marekani dhidi ya kukiuka makubaliano ya nyuklia ya Vienna na kusisitiza kuwa, endapo Washington itajiondoa kwenye mapatano hayo ya kimataifa kama inavyotishia, basi hatua hiyo itakuwa na matokeo mabaya.