Aug 02, 2017 08:04
Kila siku moja inayopita ya vita vya Saudi Arabia dhidi ya watu wa Yemen, kunadhihirika sura mpya na ya kikatili zaidi ya mauaji ya kimbari yanayofanyika nchini humo, na sasa baada ya kutumia silaha zilizopigwa marufuku kama zile za vishada kuua raia wasio na hatia wa Yemen, Aal Saud na washirika wao wanatumia silaha ya kibiolojia kufanya maangamizi ya wanadamu.