-
Waziri wa Afya Kenya: Hoteli na migahawa isiwapokee watu ambao hawajachanjwa
Dec 28, 2021 04:32Serikali ya Kenya kupitia Wizara ya Afya, imeagiza migahawa na hoteli kutotoa huduma kwa wateja ambao hawajachanjwa kama njia ya kukabiliana na maambukizi ya COVID-19 nchini humo hususan katika kipindi hiki cha sikukuu za mwishoni mwa mwaka.
-
Hafla ya ufunguzi ya somo la lugha ya Kifarsi kwa raia wa Kenya
Dec 04, 2021 23:59Hafla ya ufunguzi wa mafunzo ya lugha ya Kifarsi kwa raia wa Kenya imefanyika kwa hotuba ya Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu huko Kenya.
-
Covid-19; Wasiochanja kutopewa huduma muhimu za serikali Kenya
Nov 22, 2021 08:58Wananchi wa Kenya ambao hawajapiga dozi kamili ya chanjo ya Covid-19 watanyimwa hudumu muhimu zinazotolewa na taasisi za serikali ya nchi hiyo kuanzia mwezi ujao wa Disemba.
-
Kenya na Marekani zajadili namna ya kukomesha machafuko Sudan na Ethiopia
Nov 18, 2021 04:44Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken amekutana na kufanya mazungumzo na Rais Uhuru wa Kenyatta wa Kenya kujadili namna ya kuhitimisha machafuko katika nchi za Sudan na Ethiopia.
-
Uchumi wa Kenya wastawi kwa asilimia 10
Nov 11, 2021 04:36Uchumi wa Kenya ulistawi kwa kiwango cha asilimia 10.1 katika robo ya pili ya mwaka huu 2021.
-
Familia ya mwanamke wa Kenya aliyeuawa yalishtaki jeshi la Uingereza
Nov 10, 2021 10:54Familia ya mwanamke wa Kenya anayedaiwa kuuawa na askari wa Uingereza imelishtaki jeshi la UK ikitaka lishurutishwe kutoa majibu ya kitendawili cha mauaji hayo.
-
Miguna Miguna: Uchaguzi wa rais 2022 Kenya hautakuwa huru na wa haki
Oct 28, 2021 07:38Wakili maarufu Mkenya, Miguna Miguna amedai kuwa uchaguzi wa urais wa 2022 hautakuwa wa kuaminika na kitakachofanyika ni kutawazwa kwa mgombea mmoja.
-
Somalia yatoa wito wa kushirikiana na Kenya baada ya uamuzi wa ICJ
Oct 13, 2021 22:52Rais wa Somalia amesema katika hotuba yake aliyotoa jana Jumatano kwamba, uamuzi uliotolewa siku ya Jumanne na Mahakama ya Kimataifa ya Uadilifu (ICJ) kuhusu mzozo wa mpaka na Kenya ni fursa kwa nchi mbili hizo kushirikiana.
-
Kenya yapinga uamuzi wa ICJ kuhusu mzozo wa mpaka wa baharini na Somalia
Oct 13, 2021 09:28Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amepinga uamuzi uliotolewa jana Jumanne na Mahakama ya Kimataifa ya Uadilifu (ICJ), kuhusu mzozo wa muda mrefu wa nchi hiyo na Somalia juu ya mpaka wa baharini wa pande hizo mbili.
-
ICJ yakataa madai ya Kenya katika mzozo wa mpaka wa baharini na Somalia
Oct 12, 2021 12:41Mahakama ya UN imetoa uamuzi kwa maslahi ya Somalia katika mzozo wa muda mrefu wa nchi hiyo na Kenya juu ya mpaka wa baharini wa pande hizo mbili.