-
Kenya yataka dunia isaidie kikosi cha AMISOM kulinda amani Somalia
Sep 23, 2017 04:43Kenya imeitaka jamii ya kimataifa iongeze zaidi usaidizi wake kwa Kikosi cha Umoja wa Afrika cha Kulinda amani Somalia, AMISOM ili kiweze kushughulikia kwa kina vitisho vya usalama kabla ya kuanza kutekelezwa mpango wa kupunguza idadi ya askari wake.
-
Mwanasheria Mkuu: Kenya haiko kwenye hatari ya mgogoro wa kikatiba
Sep 22, 2017 13:08Mwanasheria Mkuu wa Kenya amesema kuwa nchi hiyo haitakabiliwa na mgogoro wa kikatiba au wa kisiasa hata kama uchaguzi rais wa marudio uliopangwa kufanyika Oktoba 26, umesogezwa tarehe hadi baada ya mwishoni mwa Oktoba.
-
Kenya yachelewesha kuanza vikao vya EALA tangu Juni 2017
Sep 22, 2017 04:34Hatua ya Kenya kutoteua wabunge wake wa Bunge la Afrika Mashariki EALA hadi sasa imechelewesha kuanza vikao vya chombo hicho cha kieneo.
-
Tarehe ya uchaguzi wa marudio Kenya yasogezwa mbele
Sep 22, 2017 04:22Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka ya Kenya (IEBC) imebadilisha tarehe ya kufanyika uchaguzi wa marudio wa urais hadi Oktoba 26 mwaka huu na wala sio Oktoba 17 kama ilivyotangaza hapo awali.
-
Rais wa Kenya: Hukumu ya Mahakama ya Juu ilikuwa ni "mapinduzi"
Sep 21, 2017 11:15Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amesema Mahakama ya Juu ya nchi hiyo ilifanya "mapinduzi" dhidi ya matakwa ya wananchi ilipobatilisha matokeo ya uchaguzi wa rais uliofanyika mwezi uliopita ambao yeye alishinda.
-
Mahakama ya Juu Kenya yatoa ufafanuzi wa kubatilisha uchaguzi wa urais
Sep 20, 2017 09:47Mahakama ya Juu nchini Kenya imesema haijuti kuchukua uamuzi wa kubatilisha ushindi wa Rais Uhuru Kenyatta katika uchaguzi mkuu uliofanyika Agosti 8 mwaka huu, huku ikiilaumu Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka IEBC kwa kuendesha zoezi hilo kinyume cha sheria.
-
Jaji Mkuu wa Kenya amtuhumu Mkuu wa Polisi kwa kupuuzia usalama wa majaji
Sep 19, 2017 23:54Jaji Mkuu wa Kenya, David Maraga amemtuhumu Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Joseph Boinett kwa kupuuzia usalama wa majaji na kwamba anahatarisha maisha yao.
-
Wafuasi wa Jubilee waandamana Kenya kupinga uamuzi wa Mahakama
Sep 19, 2017 11:23Polisi nchini Kenya wamelazimika kutumia gesi ya kutoa machozi kuwatawanya wafuasi wa chama cha Jubilee cha Rais Uhuru Kenyatta ambao walikuwa wakiandamana nje ya Mahakama ya Kilele mjini Nairobi wakipinga uamuzi wa mahakama hiyo kubatilisha uchaguzi wa rais wa Agosti 8.
-
Hatma ya kufanyika uchaguzi wa rais Kenya katika tarehe iliyopangwa bado haijajulikana hadi sasa
Sep 18, 2017 03:38Duru za habari za Magharibi zimeripoti kuwepo suitafahamu kuhusiana na tarehe ya kufanyika uchaguzi wa rais wa marudio nchini Kenya.
-
Rais Kenyatta: Nilihisi uchungu sana kwa hatua ya mahakama kufuta ushindi wangu
Sep 14, 2017 00:17Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amesema kuwa, alihisi uchungu mwingi baada ya Mahkama ya Kilele nchini humo kufuta ushindi wake katika uchaguzi uliopita wa tarehe Nane Agosti mwaka huu.