-
Mahakama ya Juu Kenya yatengua matokeo ya uchaguzi wa Rais
Sep 01, 2017 05:00Mahakama ya Juu ya Kenya imetengua matokeo ya uchaguzi mkuu uliofanyika mwezi uliopita nchini humo na kumpa ushindi Rais wa sasa wa nchi hiyo, Uhuru Kenyatta.
-
SAUTI, Mahakama Kuu Kenya yauruhusu upinzani kukagua Computer za IEBC ili kuthibitisha kama kuna wizi ulivyofanyika kwenye uchaguzi
Aug 28, 2017 12:53Kesi inayopinga matokeo ya urais nchini Kenya imeanza kusikilizwa rasmi na mahakama ya juu zaidi nchini humo hii leo, huku uapnde wa malalamiko ambao ni muungano wa upinzani ukianza utetezi wake kwa saa tano.
-
Usafirishaji bidhaa za Iran nchini Kenya kuongezeka kwa asilimia 100 katika mwaka 2017
Aug 27, 2017 10:23Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Kenya amesema usafirishaji bidhaa zisizo za mafuta za Iran kuelekea nchini Kenya katika miezi sita ya kwanza ya mwaka huu wa 2017 ulikuwa wa kiwango cha dola milioni 58 na inakadiriwa kuwa hadi ifikapo mwishoni mwa mwaka huu kiwango hicho kitaongezeka kwa kasi kubwa na kufikia asilimia 100.
-
Marufuku ya mifuko ya plastiki kutekelezwa Kenya kuanzia Agosti 28
Aug 25, 2017 01:54Serikali ya Kenya imetanagaza kwamba marufuku ya mifuko ya plastiki itaanza kutekelezwa Jumatatu Agosti 28 kama ilivyopangwa.
-
Ongezeko la asilimia 58 la bidhaa za Iran zinazouzwa Kenya
Aug 23, 2017 23:14Kumekuwa na ongezeko la asilimia 58 ya bidhaa za Jamhuri ya Kiislamu ya Iran zinazouzwa nchini Kenya katika kipindi cha miezi minne iliyopita ikilinganishwa na muda kama huo mwaka 2016.
-
Upinzani Kenya kuieleza mahakama jinsi teknolojia ilivyowezesha wizi wa kura
Aug 22, 2017 11:00Mrengo wa upinzani nchini Kenya umesema kuwa utathibitisha mbele ya Mahakama ya Kilele ya nchi hiyo kwamba teknolojia ilifanikisha kuliko kuzuia wizi wa kura wakati wa uchaguzi mkuu nchini humo hivi karibuni, ikiwa ni katika juhudi za mrengo huo za kutaka kubadilisha kura alizoshinda Rais Uhuru Kenyatta katika uchaguzi huo uliofanyika mwanzoni mwa mwezi huu.
-
Sauti, Mahojiano kuhusu kuuawa na kujisalimisha viongozi zaidi wa ash-Shabab je, kuna maana ya kundi hilo kusambaratika au la?
Aug 20, 2017 11:59Jeshi la polisi Kenya limeongeza harakati ya kamatakamata ukanda wa Pwani, baada ya kuuwawa kiongozi wa masuala ya lojistiki wa kundi la kigaidi na kitakfiri la ash-Shabab eneo bunge la Kisauni mjini Mombasa.
-
Upinzani Kenya wawasilisha mashtaka mahakamani kupinga matokeo ya uchaguzi mkuu
Aug 19, 2017 11:27Muungano wa upinzani nchini Kenya wa National Super Alliance (NASA) umewasilisha kesi ya kupinga ushindi wa Rais Uhuru Kenyatta katika uchaguzi mkuu uliofanyika tarehe 8 Agosti na kufuatiwa na malalamiko na machafuko.
-
Al-Shabaab yawakata vichwa watu 3 kaunti ya Lamu, Kenya
Aug 18, 2017 03:40Kwa akali watu watatu wameuawa kwa kukatwa vichwa na wanachama wa kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabab katika kaunti ya Lamu, pwani ya Kenya.
-
SAUTI, Raila Odinga: Naelekea mahakamani kuonyesha uchakachuaji wa IEBC ulivyofanyika kwa maslahi ya Rais Kenyatta
Aug 16, 2017 12:54Kinara wa muungano wa upinzani wa NASA nchini Kenya, Raila Odinga hatimaye amepasua mbarika na kusema kuwa ataenda katika Mahakama ya Juu ya nchi kupinga matokeo ya kura za urais yaliyompa ushindi hasimu wake Rais Uhuru Kenyatta wa chama cha Jubilee.