-
Ombi la Burundi kwa serikali ya Tanzania la kuwakamata wapinzani wake
Feb 19, 2017 23:20Katika hali ambayo juhudi za kuondokana na mgogoro wa kisiasa nchini Burundi bado zinaendelea, serikali ya Bujumbura imeiomba Tanzania kuwatia mbaroni wapinzani wake ambao wanaosakwa na mahakama za nchi hiyo, ambao kwa hivi sasa wako kaskazini mwa Tanzania.
-
Vikao vya kuupatia ufumbuzi mgogoro wa Libya na changamoto zilizopo
Feb 18, 2017 23:11Juhudi za kieneo na kimataifa za kuupatia ufumbuzi mgogoro wa Libya zingali zinaendelea huku kukiwa hakuna kikao chochote kati ya vilivyofanyika ambacho hadi sasa kimeweza kuupatia ufumbuzi mgogoro wa nchi hiyo. Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Tunisia, Algeria na Misri kwa mara nyingine tena wanatazamiwa kukutana huko Tunisia kujadili njia za kukomesha mgogoro wa miaka sita wa Libya.
-
Viongozi wa nchi za Sahel Afrika wasisitiza mapambano dhidi ya ugaidi
Feb 07, 2017 11:35Viongozi wa nchi tano za eneo la Sahel barani Afrika wametilia mkazo udharura wa kuwepo ushirikiano na kuchukuliwa hatua za haraka za kupambana na ugaidi na makundi yenye misimamo mikali katika eneo hilo.
-
Masuala ya Afrika, ajenda kuu ya kikao cha viongozi wa AU Addis Ababa
Jan 30, 2017 08:44Kikao cha 28 cha viongozi wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) kimefanyika leo Jumatatu mjini Addis Ababa Ethiopia kwa shabaha ya kujadili masuala na matatizo ya nchi za Afrika hususan migogoro ya Sudan Kusini na uchaguzi wa mkuu wa Kamisheni ya AU.
-
Uchunguzi wa changamoto za bara la Afrika katika kikao cha Bamako
Jan 13, 2017 09:43Kikao cha 27 cha viongozi wa nchi za Kiafrika na Ufaransa kimeanza leo Ijumaa huko Bamako mji mkuu wa Mali kwa shabaha ya kuchunguza masuala ya kiuchumi, migogoro ya Kisasa na kiusalama yanayolikabili bara la Afrika.
-
Kamisheni ya pamoja ya JCPOA yachunguza ukiukaji ahadi wa Marekani
Jan 11, 2017 03:39Kikao cha kamisheni ya pamoja ya Iran na kundi la 5+1 katika kiwango cha Manaibu Mawaziri wa Mashauri ya Kigeni kilichoitishwa kwa takwa la Dakta Muhammad Javad Zarif Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu kwa ajili ya kujadili ukiukaji wa makubaliano hayo uliofanywa na Marekani kimemalizika huko Vienna Austria kwa kutolewa taarifa.
-
Kujadiliwa changamoto za eneo la katikati mwa Afrika katika mkutano wa Yaounde Cameroon
Dec 27, 2016 11:30Kikao cha dharura cha wakuu wa nchi za eneo la katikati mwa Afrika kilichokuwa kikifanyika katika mji mkuu wa Cameroon Yaounde kimemalizika kwa washiriki kusisitiza juu ya udharura wa kukabiliana na changamoto za kiuchumi zinazolikabili eneo hilo.
-
Kikao cha viongozi wa IGAD cha kujadili amani ya eneo
Dec 11, 2016 03:38Viongozi wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Ustawi wa Mashariki mwa Afrika IGAD wamekutana katika mji mkuu wa Ethiopia, Addis Ababa kwa kikao cha 29 cha dharura ambacho kimefanyika kwa uenyekiti wa Waziri Mkuu wa nchi hiyo Hailemariam Desalegn kujadili amani na uthabiti wa eneo hasa katika nchi za Sudan Kusini na Somalia.
-
Kivuli cha migogoro ya kisiasa katika kikao cha kimataifa cha nchi zinazozungumza lugha ya Kifaransa
Nov 26, 2016 10:09Kikao cha Kimataifa cha 16 cha Nchi Zinazozungumza lugha ya Kifaransa kinafanyika huko Madagascar lengo likiwa ni kuchunguza migogoro ya kisiasa ya nchi hizo. Marais wa nchi au Mawaziri Wakuu zaidi ya 30 kutoka nchi 80 zinazozungumza lugha ya Kifaransa wanashiriki katika kikao hicho.
-
Kikao cha nne cha viongozi wa Kiarabu na Kiafrika na changamoto zake
Nov 25, 2016 02:29Kikao cha nne cha pamoja baina ya viongozi wa Kiarabu na Kiafrika kimefanyika katika anga ya kushadidi tofauti na mivutano ya kisiasa baina ya pande mbili.