Mkutano wa 3 wa Kimataifa wa Mshikamano na Watoto na Vijana wa Palestina kwa ajili ya kumkumbuka shahidi Muhammad al Durrah umefanyika hapa Tehran.
Spika wa Bunge la Iran amesema kuwa Rais Donald Trump wa Marekani amekosea kufananisha medani ya siasa za uwanja wa michezo ya kuigiza na hatua hii inatoa pigo kwa hadhi ya taifa la Marekani.
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH limesambaza mkanda wa video na sauti wakati jeshi hilo lilipotoa onyo kwa Manuwari ya Kifalme wa Uingereza kwamba ikae mbali na isiingilie operesheni ya kusimamishwa meli ya mafuta iliyokuwa inapeperushwa bendera ya Uingereza katika eneo la Ghuba ya Uajemi.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza juu ya stratijia ya Tehran ya kuinua kiwango cha usalama katika Mashariki ya Kati na kusema kwamba, usalama wa eneo hili unaweza kuletwa na nchi husika za eneo hili na si vinginevyo.
Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu, Bunge la Iran, amesema sera za Saudi Arabia na Imarati (UAE) zitawadhuru katika siku za usoni.
Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amekosoa vikali njama za nchi za Magharibi zikiongozwa na Marekani zilizopewa jina la 'Muamala wa Karne' dhidi ya Wapalestina, huku akitoa mwito wa mahudhurio makubwa katika maandamano ya Siku ya Kimataifa ya Quds.
Spika wa Bunge la Iran, Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu, Ali Larijani amesema Wairani kamwe hawatasalimu amri mbele ya wanaotumia mabavu na kuongeza kuwa: "Wakuu wa Marekani wanapaswa kufahamu kuwa, Iran ni mshindani mgumu kwao."
Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) Ali Larijani ameeleza kusikitishwa kwake na hatua ya nchi za Kiislamu ya kuitelekeza na kuiweka pembeni kadhia muhimu katika ulimwengu wa Kiislamu hivi sasa, ambayo ni Palestina.
Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu, Bunge la Iran, Ali Larijani amesema: "Kwa vikwazo vyake vya kiuchumi dhidi ya serikali na taifa la Iran, Marekani inatekeleza ugaidi wa kiuchumi."
Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran amelaani matamshi ya kichochezi ya rais wa Marekani kwamba utawala wa Kizayuni wa Israel una mamlaka ya kulimiliki eneo la Golan la Syria unalolikalia kwa mabavu.