-
Wasichana wahajiri wa Kiafrika wananajisiwa na hata kupewa ujauzito katika kambi ya EU, Libya
Jun 21, 2021 08:12Kundi la wasichana wahamiaji waliowekwa katika kituo kinachosimamiwa na serikali ya Libya wamewashutumu walinzi wa kituo hicho, kinachofadhiliwa na Umoja wa Ulaya, kwamba wanawabaka na kuwanyanyasa kingono.
-
Mangoush: Libya haitaruhusu ardhi yake itumiwe dhidi ya nchi nyingine
Jun 11, 2021 22:21Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa nchini Libya amesema kuwa nchi yake haitakubali kutumiwa kama kituo cha kuvuruga amani na utulivu katika kanda hiyo ya Afrika au kutumiwa ardhi na anga yake dhidi ya upande wowote mwingine.
-
Sisitizo la Macron kuhusu kusitishwa uingiliaji wa kigeni nchini Libya
Jun 03, 2021 08:57Katika hali ambayo kunafanyika jitihada za kuhitimisha mgogoro wa Libya ili uchaguzi utakaoyashirikisha makundi yote ya kisiasa ufanyike, uwepo wa wanajeshi wa kigeni na uingiliaji wa madola ajinabi katika mchakato wa amani nchini humo vinatambuliwa kuwa ni kizuizi katika kufikia amani ya kudumu.
-
Mkuu wa Baraza la Uongozi la Libya akutana na Rais wa Tunisia
May 31, 2021 02:53Mkuu wa Baraza la Uongozi la Libya amehimiza kurahishishwa mawailiano na sekta ya uchukuzi baina ya nchi yake na Tunisia.
-
Mjumbe wa UN: Mamluki walioko Libya ni tishio kwa Afrika ya Kaskazini
May 22, 2021 22:19Mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Libya ametahadharisha katika kikao cha Baraza la Usalama kwamba mchakato muhimu wa kuwaondoa mamluki na wapiganaji wa kigeni kutoka Libya umekwama na kwamba kuendelea kuwapo kwao nchini humo ni tishio sio tu kwa Libya bali kwa eneo zima la Kaskazini mwa Afrika.
-
EU yajipanga kutoa misaada kwa Libya na Tunisia ili kuzuia wahajiri wasielekee Ulaya
May 20, 2021 23:07Kamishna wa Mambo ya Ndani katika Umoja wa Ulaya (EU) Ylva Johansson, amesema umoja huo unashauriana na Tunisia na Libya ili kufikia mapatano yatakayowezesha kuzuia wahajiri wasielekee barani ya Ulaya.
-
Katibu Mkuu wa UN: Wapiganaji wa kigeni wangaliko Libya, ni ukiukaji wa usitishaji vita
May 15, 2021 09:17Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema, wapiganaji wa kigeni na mamluki wangali wako nchini Libya, ukiwa ni ukiukaji wa mapatano ya kusitisha mapigano yaliyofikiwa mwaka jana; na akatoa mwito waondolewe nchini humo na kukomeshwa pia ukiukaji wa vikwazo vya silaha vilivyowekwa na Umoja wa Mataifa.
-
Baraza Kuu la utawala Libya lalaani uingiliaji wa nchi za Magharibi katika mchakato wa uchaguzi
May 08, 2021 21:43Baraza Kuu la Serikali ya Libya limelaani uingiliaji kati wa nchi za Magharibi katika mchakato wa uchaguzi mkuu nchini humo.
-
Takwa na sisitizo la kuondoka vikosi vya kigeni nchini Libya
May 04, 2021 21:41Baada ya kupita miezi kadhaa tangu kuanza mwenendo wa amani nchini Libya na kuweko juhudi kubwa za kuitisha uchaguzi wa nchi hiyo baadaye mwaka huu, uwepo wa vikosi vya kigeni na vituo vyao vya kijeshi kumeendelea kuwa kikwazo katika njia hiyo.
-
Al-Mushiri: Haftar ni tishio kwa uchaguzi mkuu wa Libya
May 01, 2021 22:35Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Libya amesema kutosalimu amri kwa kamanda wa linalojiita jeshi la taifa mbele ya mamlaka au sheria yoyote ni tishio kwa chaguzi zijao za Bunge na Rais.