-
Antonio Guterres: Mustakbali wa Libya upo hatarini
Oct 06, 2020 08:42Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ameyahimiza mataifa makubwa duniani yenye maslahi katika vita vinavyoendelea huko Libya kuacha kuzitumia silaha serikali waitifaki wao.
-
Libya na Uturuki zasisitiza kuhusu uhusiano wa karibu
Oct 05, 2020 06:07Rais Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki amekutana na Waziri Mkuu wa Libya anayeondoka Fayez al-Sarraj, ambaye anaongoza Serikali ya Mwafaka wa Kitaifa (GNA), inayotambuliwa na Umoja wa Mataifa.
-
Duru ya pili ya mazungumzo baina ya pande hasimu Libya yaanza nchini Morocco
Oct 03, 2020 04:19Duru ya pili ya mazungumzo baina ya pande hasimu nchini Libya imeanza katika katika mji wa Bouznika huko nchini Morocco ikiwa ni katika juhudi za kujaribu kuutafutia ufumbuzi mgogoro wa nchi hiyo.
-
UN: Mazungumzo ya amani Libya yamalizika; Imarati bado yatuma silaha kimagendo
Sep 30, 2020 23:01Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa mazungumzo ya makundi mbalimbali ya Libya ya kutafuta amani ya nchi yao yamemalizika nchini Misri na matokeo ya mazungumzo hayo ni mazuri.
-
Wahajiri 16 wafariki dunia baada ya boti yao kughariki pwani ya Libya
Sep 26, 2020 08:44Watu wasiopungua 16 wamefariki dunia katika Bahari ya Mediterania baada ya boti yao kuzama, huko pwani ya Libya.
-
Uturuki: Ankara itaendelea kuisaidia serikali ya GNA Libya hata baada ya Sarraj kung'atuka
Sep 21, 2020 23:11Uturuki imetangaza kuwa itaendelea kuiunga mkono serikali inayotambuliwa kimataifa ya Libya licha ya Waziri Mkuu Fayez al-Sarraj kutangaza wiki iliyopita kwamba, anapanga kuondoka madarakani mwishoni mwa mwezi ujao.
-
Sisitizo la Umoja wa Mataifa la kutekelezwa vikwazo vya silaha dhidi ya Libya
Sep 17, 2020 22:12Hali ya wasiwasi kuhusu mgogoro wa kisiasa unaoikabili Libya na hali inayolegalega nchini humo ni mambo ambayo yangali yanaendelea kushuhudiwa licha ya kutangazwa usitishaji vita nchini humo. Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limepasisha azimio na kutaka kutekelezwa vikwazo vya silaha dhidi ya Libya na kuondolewa mamluki wote katika nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika.
-
Waziri Mkuu wa GNA Libya kung'atuka madarakani ifikapo mwishoni mwa Oktoba
Sep 17, 2020 08:39Waziri Mkuu wa Serikali ya Muafaka wa Kitaifa ya Libya GNA amesema, atajiuzulu wadhifa wake huo na kukabidhi hatamu za madaraka kwa uongozi mpya utakaochaguliwa kupitia kamati ya mazungumzo ya amani.
-
Katibu Mkuu wa UN kumteuwa mjumbe maalumu katika masuala ya Libya
Sep 16, 2020 22:31Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limemuomba Katibu Mkuu wa umoja huo Antonio Guterres kufanya uteuzi wa Mjumbe Maalumu ili kusuluhisha mzozo unaoendelea nchini Libya na kuongoza jitihada za kurejesha amani katika nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika.
-
UN yataka kutekelezwa vikwazo vya silaha dhidi ya Libya
Sep 16, 2020 03:17Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limepasisha azimio la kutekeleza vikwazo vya silaha dhidi ya Libya na kuondoka mamluki wote katika nchi hiyo ya Kiafrika.