-
Serikali ya umoja wa kitaifa ya Libya yamfuta kazi waziri wake wa Ulinzi
Jul 30, 2018 09:49Rais wa serikali ya umoja wa kitaifa ya Libya amemfuta kazi Waziri wa Ulinzi wa nchi hiyo kwa kile kilichotajwa kuwa kuhusika katika shambulio dhidi ya kituo cha anga magharibi mwa nchi hiyo.
-
Benki ya dunia yatahadharisha kuhusu taathira za magendo ya mafuta huko Libya
Jul 28, 2018 03:42Benki ya Dunia imetangaza kuwa uchumi wa Libya umepata hasara kubwa kutokana na kuibiwa mafuta ya nchi hiyo kuelekea nchi jirani hususan huko Tunisia.
-
Vita vya kuwania ngawira Libya vyapamba moto baina ya Ufaransa na Italia
Jul 21, 2018 22:58Mtandao wa habari wa Algeria umefichua kuwa Ufaransa na Italia zinachuana vikali kuwania ngawira zaidi huko Libya na kwamba wakati mwingine mchuano huo unafikia kiwango cha mapigano na vita vya kisiasa.
-
Wahajiri 8 wakiwemo watoto 6 waaga dunia kwenye kontena Libya
Jul 17, 2018 02:36Wahajiri wanane wakiwemo watoto sita wamepoteza maisha baada ya kuishiwa na hewa wakiwa ndani ya kasha la kusafirishia mizigo katika mji wa Zuwara ulioko katika pwani ya magharibi mwa Libya.
-
Mjumbe wa UN nchini Libya: Mamluki maajinabi wanataka kuzidhibiti vyanzo vya mafuta vya nchi hiyo
Jul 16, 2018 22:21Mjumbe wa Umoja wa Mataifa anayeshughulikia mgogoro wa Libya amesema kuhusu matukio ya hivi karibuni nchini humo kuwa mamluki kutoka nchi ajinabi wanajaribu kudhibiti mafuta ya Libya.
-
EU yafungua ubalozi wake wa Libya uliofungwa 2014
Jul 15, 2018 02:37Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya, Federica Mogherini ameitembelea Tripoli, mji mkuu wa Libya na kufungua upya ubalozi wa umoja huo uliohamishiwa Tunis, mji mkuu wa Tunisia mwaka 2014.
-
Mashambulizi ya NATO Libya, yamewaletea raia wa nchi hiyo aina kadhaa za saratani
Jul 14, 2018 23:18Nouri al-Daruqi, Mtafiti wa nchini Libya amesema kuwa aina kadhaa za ugonjwa wa saratani zimeibuka baada ya Muungano wa Kijeshi wa Nchi za Magharibi (NATO) kuishambulia kijeshi nchi hiyo mwaka 2011.
-
Wafanyakazi wauawa katika kituo cha maji nchini Libya
Jul 07, 2018 09:10Wabeba silaha wasiojulikana wamewapiga risasi na kuwaua wafanyakazi wawili na kuwateka nyara wengine wawili katika kituo cha kusambaza maji kusini mashariki mwa Libya mapema leo asubuhi. Shambulizi hilo ni la pili kulenga vituo vya kusambaza maji nchini humo katika kipindi cha siku mbili zilizopita.
-
ICC yatoa waranti nyingine ya kukamatwa kamanda wa jeshi la Libya
Jul 05, 2018 08:58Kwa mara nyingine tena, majaji wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) wametoa waranti ya kutiwa nguvuni kamanda wa Jeshi la Taifa la Libya (LNA) anayetuhumiwa kuua makumi ya wafungwa wa kitakfiri.
-
Wahajiri 63 wahofiwa kufa maji baada ya boti yao kuzama pwani ya Libya
Jul 03, 2018 11:07Wahajiri 63 wametoweka baada ya boti yao kuzama katika pwani ya Libya, wakiwa katika jitihada za kuvuka bahari ya Mediterranean na kuingia barani Ulaya kutafuta maisha.