-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Italia atahadharisha kuenea ghasia za Ufaransa katika nchi nyingine
Jul 04, 2023 04:25Waziri wa Mambo ya Nje wa Italia amesisitiza kuwa nchi za Ulaya zinapasa kubuni sera ili kuzuia machafuko yaliyoigubika Ufaransa kuenea katika nchi nyingine.
-
Ghasia zashtadi Senegal, mitandao ya kijamii yafungwa
Jun 03, 2023 01:34Watu kadhaa wameuawa huku wengine wengi wakijeruhiwa nchini Senegal, katika maandamano ya ghasia ya wafuasi wa kiongozi wa upinzani nchini humo Ousmane Sonko, ambaye karibuni alihukumiwa kifungo cha miaka miwili jela.
-
Raila Odinga kuanza tena maandamano dhidi ya serikali ya Kenya
Apr 24, 2023 12:35Mrengo wa upinzani nchini Kenya umesema kuwa umepanga kuanza tena maandamano dhidi ya serikali kuanzia tarehe Pili mwezi ujao wa Mei; ikiwa zimepita karibu wiki tatu tangu usimamishe maandamano yake dhidi ya serikali ya Rais William Ruto ili kutoa fursa ya kushiriki kwenye mazungumzo na serikali.
-
Ombi la watu wa Morocco la kufutwa uhusiano wa nchi yao na utawala wa Kizayuni wa Israel
Apr 03, 2023 03:23Kwa mnasaba wa Machi 30, Siku ya Ardhi ya Palestina, idadi kubwa ya raia wa Morocco walijumuika katika mji mkuu, Rabat na kushiriki katika maandamano ya kupinga utawala wa Kizayuni wa Israel, ambapo kwa mara nyingine wametaka kufutwa kwa mapatano ya kuanzishwa uhusiano wa kawaida kati ya serikali yao na utawala huo dhalimu.
-
Maandamano ya kutaka kufungwa kampuni za silaha za Israel yafanyika UK
Apr 02, 2023 11:16Wanaharakati wa kutetea haki za wananchi madhulumu wa Palestina wamefanya maandamano katika miji kadhaa ya Uingereza, kushinikiza kufungwa kwa mashirika ya kuzalisha silaha ya utawala wa Kizayuni wa Israel katika nchi hiyo ya Ulaya.
-
Wananchi wa Morocco waandamana kupinga nchi yao kuwa na uhusiano wa kawaida na Israel
Apr 01, 2023 09:19Maelfu ya wananchi wa Morocco wameandamana na kutangaza upinzani wao dhidi ya hatua ya nchi hiyo ya kuanzisha uhusiano wa kawaida na utawala haramu wa Israel unaofanya mauaji kila siku huko Palestina.
-
Netanyahu alegeza kamba baada ya maji kumfika shingoni
Mar 28, 2023 07:29Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel, Benjamin Netanyahu amelazimika kuakhirisha utekelezaji wa mpango wake wa kile kinachoitwa 'mageuzi ya mahakama' kufuatia maandamano ya Wazayuni dhidi ya mpango huo kwa wiki 12 mfululizo.
-
Netanyahu akaribishwa UK kwa maandamano ya kuwaunga mkono Wapalestina
Mar 25, 2023 08:06Mamia ya waungaji mkono wa Palestina na wapinzani wa utawala haramu wa Israel wamefanya maandamano mjini London, kulaani safari ya Waziri Mkuu wa utawala huo wa Kizayuni, Benjamin Netanyahu nchini Uingereza.
-
Waungaji mkono wa Rais wa Tunisia waandamana dhidi ya 'wasaliti'
Mar 21, 2023 02:27Mamia ya wafuasi wa serikali ya Rais Kais Saied wa Tunisia jana Jumatatu walifanya maandamano katika mji mkuu Tunis, kuonyesha uungaji mkono wao kwa kiongozi huyo anayekabiliwa na mashinikizo ya kumtaka ajiuzulu.
-
Kadhaa wajeruhiwa na kukamatwa katika maandamano ya wapinzani Kenya, Afrika Kusini
Mar 20, 2023 14:01Maafisa usalama nchini Kenya wametumia mabomu ya gesi ya kutoa machozi na maji ya kuwasha kukabiliana na wafuasi wa kinara wa upinzani nchini humo Raila Odinga, ambao wamejitokeza kwa wingi kushiriki maandamano ya nchi nzima dhidi ya serikali ya Rais William Ruto.