-
Maelfu waandamana Niger wakitaka kufukuzwa askari wa US, Ufaransa
Aug 03, 2023 23:27Maelfu ya wananchi wa Niger wamefanya maandamano katika mji mkuu Niamey, wakitaka kufukuzwa nchini humo mara moja wanajeshi wa Marekani na Ufaransa.
-
Waislamu Nigeria waandamana kulaani kuchomwa moto Qurani
Jul 27, 2023 06:51Waislamu nchini Nigeria wamefanya maandamano kulaani vitendo vya mara kwa mara vya kuvunjiwa heshima Qur'ani Tukufu katika nchi za Ulaya.
-
Wairaqi walaani njama za Marekani za kutaka kuwaua viongozi wa muqawama
Jul 15, 2023 03:18Wananchi wa Iraq wamefanya maandamano katika mji mkuu Baghdad, kupinga na kulaani uingiliaji wa Marekani katika masuala ya ndani ya nchi hiyo, na vile vile njama za Washington za kutaka kuwaua kigaidi viongozi wa kambi ya muqawama nchini humo.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Italia atahadharisha kuenea ghasia za Ufaransa katika nchi nyingine
Jul 04, 2023 00:55Waziri wa Mambo ya Nje wa Italia amesisitiza kuwa nchi za Ulaya zinapasa kubuni sera ili kuzuia machafuko yaliyoigubika Ufaransa kuenea katika nchi nyingine.
-
Ghasia zashtadi Senegal, mitandao ya kijamii yafungwa
Jun 02, 2023 22:04Watu kadhaa wameuawa huku wengine wengi wakijeruhiwa nchini Senegal, katika maandamano ya ghasia ya wafuasi wa kiongozi wa upinzani nchini humo Ousmane Sonko, ambaye karibuni alihukumiwa kifungo cha miaka miwili jela.
-
Raila Odinga kuanza tena maandamano dhidi ya serikali ya Kenya
Apr 24, 2023 09:05Mrengo wa upinzani nchini Kenya umesema kuwa umepanga kuanza tena maandamano dhidi ya serikali kuanzia tarehe Pili mwezi ujao wa Mei; ikiwa zimepita karibu wiki tatu tangu usimamishe maandamano yake dhidi ya serikali ya Rais William Ruto ili kutoa fursa ya kushiriki kwenye mazungumzo na serikali.
-
Ombi la watu wa Morocco la kufutwa uhusiano wa nchi yao na utawala wa Kizayuni wa Israel
Apr 02, 2023 23:53Kwa mnasaba wa Machi 30, Siku ya Ardhi ya Palestina, idadi kubwa ya raia wa Morocco walijumuika katika mji mkuu, Rabat na kushiriki katika maandamano ya kupinga utawala wa Kizayuni wa Israel, ambapo kwa mara nyingine wametaka kufutwa kwa mapatano ya kuanzishwa uhusiano wa kawaida kati ya serikali yao na utawala huo dhalimu.
-
Maandamano ya kutaka kufungwa kampuni za silaha za Israel yafanyika UK
Apr 02, 2023 07:46Wanaharakati wa kutetea haki za wananchi madhulumu wa Palestina wamefanya maandamano katika miji kadhaa ya Uingereza, kushinikiza kufungwa kwa mashirika ya kuzalisha silaha ya utawala wa Kizayuni wa Israel katika nchi hiyo ya Ulaya.
-
Wananchi wa Morocco waandamana kupinga nchi yao kuwa na uhusiano wa kawaida na Israel
Apr 01, 2023 05:49Maelfu ya wananchi wa Morocco wameandamana na kutangaza upinzani wao dhidi ya hatua ya nchi hiyo ya kuanzisha uhusiano wa kawaida na utawala haramu wa Israel unaofanya mauaji kila siku huko Palestina.
-
Netanyahu alegeza kamba baada ya maji kumfika shingoni
Mar 28, 2023 03:59Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel, Benjamin Netanyahu amelazimika kuakhirisha utekelezaji wa mpango wake wa kile kinachoitwa 'mageuzi ya mahakama' kufuatia maandamano ya Wazayuni dhidi ya mpango huo kwa wiki 12 mfululizo.