-
Mwendesha-mashtaka wa ICC Karim Khan aondolewa kufuatia tuhuma za unyanyasaji wa kingono
Jul 25, 2026 02:58Mkutano wa Nchi Wanachama wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) umepiga kura ya kumwondoa Mwendesha Mashtaka Karim Khan kufuatia madai ya utovu wa nidhamu wa kingono; timu yake ya wanasheria imethibitisha hayo, huku ikidokeza kuwa hatua hiyo ilikuwa ya "kisiasa".
-
Waghana waiomba ICC kuchunguza ukatili wa chuki dhidi ya wageni nchini Afrika Kusini
Jul 24, 2026 02:48Raia wawili wa Ghana wamewasilisha ombi kwa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) wakiitaka kufungua uchunguzi wa awali kuhusu vitendo vya ukatili vinavyowalenga wageni nchini Afrika Kusini, wakisema kwamba muundo, ukubwa na kukaririwa mashambulizi yanayowalenga wahamiaji vinaweza kuwa uhalifu dhidi ya ubinadamu.
-
EU yaunga mkono ICC, yapinga kampeni ya Trump ya kuvunja mahakama ya uhalifu wa kivita
Jul 16, 2026 02:55Umoja wa Ulaya (EU) umesisitiza tena uungaji mkono wake kwa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC), ukipinga kampeni mpya ya utawala wa Rais wa Marekani, Donald Trump ya kudhoofisha mahakama hiyo yenye makao yake makuu The Hague nchini Uholanzi.
-
ICC 'yahofia' kuhusu kujiondoa kwa Mali, Burkina Faso na Niger
Jul 02, 2026 11:35Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) imeeleza wasiwasi wake kuhusu kujiondoa Mali, Burkina Faso na Niger kwenye mahakama hiyo, ikisema kunadhoofisha harakati za kimataifa za kutafuta haki.
-
ICC yamsimamisha Kazi Mwendesha Mashtaka Mkuu kwa tuhuma za utovu wa nidhamu wa kingono
Jun 09, 2026 09:48Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) imemsimamisha kazi Mwendesha Mashtaka Mkuu, Karim Khan, kwa madai ya utovu wa nidhamu wa kingono na msaidizi wake.
-
ICC: Vikwazo vya US ni 'hujuma' dhidi ya haki duniani
Dec 19, 2025 07:43Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) imelaani vikwazo vya hivi karibuni vya Marekani dhidi ya majaji wawili wa korti hiyo ya Umoja wa Mataifa.
-
Mwendesha Mashtaka wa ICC aikosoa Marekani kwa kuwafananisha majaji wa mahakama hiyo na magaidi, walanguzi wa dawa za kulevya
Dec 06, 2025 10:27Naibu mwendesha mashtaka wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) ameikosoa vikali serikali ya Marekani kwa kuwawekea vikwazo majaji wa mahakama hiyo ya kimataifa, hatua ambayo amesema inaakisi jinsi Washington inavyowalenga magaidi na wafanyabiashara wa dawa za kulevya.
-
ICC yazitaka nchi wanachama kutekeleza hati za kukamatwa Netanyahu, Gallant
Oct 08, 2025 23:43Msemaji wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC), Fadi El Abdallah ameiambia kanali ya Al-Jazeera kwamba, nchi wanachama wa Mkataba wa Roma zina wajibu wa kisheria kushirikiana na mahakama hiyo katika kutekeleza waranti wa kukamatwa Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu na aliyekuwa Waziri wa Vita wa utawala huo pandikizi, Yoav Gallant.
-
ICC yamtia hatiani kiongozi wa kwanza wa wanamgambo wa Darfur kwa uhalifu wa kivita
Oct 07, 2025 02:39Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC jana Jumatatu ilimtia hatiani kiongozi wa kwanza wa wanamgambo wa Janjaweed aliyepandishwa kizimbani akihusishwa na ukatili na jinai zilizofanyika katika jimbo la Darfur nchini Sudan zaidi ya miaka 20 iliyopita.
-
ICC: Vikwazo vya US ni hujuma dhidi ya mamilioni ya wahanga wa jinai
Aug 21, 2025 02:13Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) imetumia maneno makali kuilaani Marekani, kwa hatua yake ya hivi karibuni ya kuwawekea vikwazo majaji wa mahakama hiyo, kutokana na juhudi zao za kuwafungulia mashitaka maafisa Marekani na Israel wanaotuhumiwa kuhusika na uhalifu wa kivita na aina nyingine za ukatili.