Apr 24, 2019 06:28
Mapigano nchini Libya hasa katika mji wa Tripoli na pambizoni mwake yanakuwa makali siku baada ya siku. Duru za kijeshi za Serikali ya Umoja wa Kitaifa zimetangaza kuwa, vikosi vyake vimefanikiwa kudhibiti sehemu kubwa ya uwanja wa ndege wa Tripoli. Hata hivyo wapiganaji wa Jenerali Khalifa Haftar wamedai kuwa wamekaribia mno kuingia katikati ya Tripoli.