-
Sisitizo la Putin la kuimarisha ushirikiano wa kijeshi kati ya Russia na China kwa ajili ya kukabiliana na mashinikizo ya kijiopolitiki
Dec 31, 2022 07:50Rais Vladimir Putin wa Russia jana Ijumaa aliwasiliana kwa njia ya video na Rais Xi Jinping wa China na kuashiria mapambano ya Beijing na Moscow mkabala wa mashinikizo ya kijiopolitiki na kueleza kuwa ushirikiano wa nchi mbili unasaidia kuwepo mfumo wa kiadilifu duniani.
-
China: Marekani ndiyo chanzo cha kuvurugika amani ya eneo ikiwemo Bahari ya Kusini ya China
Dec 30, 2022 22:42Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China amesema, Marekani ndiyo chanzo cha kuvurugikka amani katika eneo, ikiwa ni pamoja na Bahari ya Kusini ya China, na akaitaka Washington iache hatua zake hatarishi na za kichochezi.
-
Jibu kali la Moscow kwa tishio la Marekani la kumuua Putin
Dec 28, 2022 22:54Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Russia amesema kuwa matamshi ya maafisa wa Marekani katika Wizara ya Ulinzi ya nchi hiyo Pentagon, kuhusu pigo la kukata kichwa cha Kremlin kwa hakika ni tishio la kutaka kumuua kigaidi Rais wa Russia.
-
Zaidi ya watoto 6,000 ni wahanga wa ukatili wa bunduki nchini Marekani mwaka 2022
Dec 28, 2022 04:33Mtandao wa Hifadhi ya Ukatili wa Silaha nchini Marekani uliripoti kwamba mwaka huu unaomalizika wa 2022, zaidi ya watoto 6,000 wa nchi hiyo waliuawa au kujeruhiwa kwa kupigwa risasi na vurugu za kutumia silaha, idadi ambayo ni kubwa zaidi kuwahi kurekodiwa katika kipindi cha miaka 9 iliyopita.
-
Medvedev atabiri kugawanyika Marekani, Ulaya; Elon Musk kuwa rais wa Marekani mwaka 2023
Dec 28, 2022 00:54Dmitry Medvedev, Naibu Mwenyekiti wa Baraza la Usalama wa Taifa la Russia, amewasilisha utabiri wake wa mwaka mpya wa 2023 unaojumuisha hatima mbaya kwa Merekani na Umoja wa Ulaya, ambazo zimekuwa kwenye mzozo mkali na Russia tangu kuanza kwa vita nchini Ukraine tarehe 14 Februari mwaka huu.
-
Indhari ya Rais wa Venezuela kuhusu kufikia ubeberu wa Marekani katika hatua hatarishi zaidi
Dec 27, 2022 22:27Rais Nicolas Maduro wa Venezuela ametahadharisha kuwa ubeberu wa Marekani umeingia katika hatua hatarishi zaidi na unajaribu kufanya kila njia ili kuzusha mapigano na kuwasha moto wa vita duniani.
-
China: Mazungumzo ya JCPOA yapo katika marhala ya mwisho
Dec 27, 2022 03:56China imesema mazungumzo ya kujaribu kuhuisha makubaliano ya nyuklia ya JCPOA yapo katika hatua ya mwisho, na kusisitiza kwamba fursa ya kufufua mapatano hayo ya kimataifa ingalipo.
-
Moscow yatoa onyo baada ya Washington kutishia kumuua Rais wa Russia
Dec 27, 2022 03:50Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia ametoa indhari baada ya maafisa 'wasiojulikana' wa Wizara ya Ulinzi ya Marekani (Pentagon) kutoa vitisho vya kumuua Rais Vladimir Putin wa nchi hiyo.
-
Rais wa Venezuela: Ubeberu wa Marekani umefikia kwenye hatua hatarishi zaidi
Dec 25, 2022 22:48Rais Nicolás Maduro wa Venezuela ametahadharisha kuwa ubeberu wa Marekani umeingia katika hatua hatarishi zaidi na unajaribu kufanya kila njia ili kuzusha mapigano na kuwasha moto wa vita duniani.
-
Putin: Nina uhakika wa asilimia 100 tutayateketeza makombora ya Marekani ya Patriot Ukraine
Dec 25, 2022 22:47Rais Vladimir Putin wa Russia amesema kuhusu uamuzi wa Marekani wa kutuma mitambo ya makombora aina ya Patriot nchini Ukraine, kwamba ana uhakika wa asilimia 100 vikosi vya jeshi la nchi yake vitayateketeza makombora hayo ya ulinzi wa anga ya Washington.