-
Theluthi mbili ya wanaoamini Mungu Marekani: Corona ni ujumbe unaotoka kwa Mungu
May 17, 2020 03:30Matokeo ya uchunguzi mpya wa maoni uliofanywa nchini Marekani yanaonyesha kuwa, baada ya kuzuka mripuko wa maradhi ya Covid-19, zaidi ya asilimia 65 ya raia wa nchi hiyo wanaoamini Mungu wamefikia hitimisho kuwa Mwenyezi Mungu anawahutubu kwamba wabadilike katika maisha yao.
-
Ombi la Umoja wa Mataifa kuhusu kuondolewa vikwazo dhidi ya Iran
May 17, 2020 02:17Baada ya serikali ya Rais Donald Trump kujiondoa katika mapatano ya nyuklia ya Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji (JCPOA) mwaka 2018 katika fremu ya sera za mashinikizo ya juu kabisa na kisha kushadidisha vikwazo ambavyo havijawahi kushuhudiwa katika historia dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na licha ya kuibuka ugonjwa wa COVID-19 nchini Iran, lakini bado Trump anasisitiza kuendeleza vikwazo vyake vilivyo dhidi ya ubinadamu dhidi ya taifa hili.
-
Marekani yaiwekea Huawei vikwazo vipya, uhusiano na China wazidi kuharibika
May 16, 2020 03:09Serikali ya Marekani imeliwekea vikwazo vipya shirika kubwa la kiteknolojia la China Huawei na hivyo kupelekea uhusiano wake na China ambao umezorota kuwa mbaya zaidi.
-
Vitisho vikubwa vya Trump kwa China; upayukaji au kampeni za uchaguzi?
May 16, 2020 02:05Tangu alipoingia madarkani Donald Trump huko Marekani, rais huyo mwenye majigambo mengi amekuwa akifuata siasa maalumu dhidi ya China na kuishinikiza Beijing katika pande mbalimbali.
-
Marekani ya Trump; nembo na mshirika wa ugaidi wa kiserikali ulimwenguni
May 15, 2020 21:58Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, Marekani ni nembo ya ugaidi wa kiserikali na kueleza kwamba, historia ya nchi hiyo katika kuunga mkono ugaidi iko wazi kabisa.
-
Trump: Sitaki kuzungumza na Rais Xi, huenda tutakata uhusiano wetu na China
May 15, 2020 08:00Rais Donald Trump wa Marekani amesema haoni umuhimu wowote wa kufanya mazungumzo na mwenzake wa China, Xi Jinping, kauli ambayo inaweka bayana kuzidi kuharibika uhusiano wa Washington na Beijing wakati huu wa janga la kimataifa la corona.
-
Wapalestina wakusanyika Nablus, Ufukwe wa Magharibi kupinga safari ya Pompeo
May 15, 2020 03:40Wananchi wa Palestina wamekusanyika katika mji wa Nablus ulioko kaskazini mwa Ufukwe wa Magharibu wa Mto Jordan kupinga safari ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Mike Pompeo katika ardhi zao zinazokaliwa kwa mabavu zilizopewa jina la 'Israel'.
-
Amnesty yaikosoa Marekani kwa kuungo mkono uporaji wa ardhi za Wapalestina
May 14, 2020 19:58Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limekosoa vikali hatua ya Marekani ya kuunga mkono uamuzi wa utawala wa Kizayuni wa kulinyakua eneo la Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan na kuliunganisha na ardhi zingine unazozikalia kwa mabavu za Palestina (Israel).
-
Corona; dhihirisho la tabia ya kigaidi ya Marekani dhidi ya taifa la Iran
May 14, 2020 19:54Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, licha ya kuwa siku zote Marekani inajulikana kuwa ni nchi ya kigaidi, lakini si kwa kiwango hiki cha hata kuzuia bidhaa za afya na tiba zikiwemo dawa kuwafikia watu wa Iran.
-
Rais Rouhani: Utawala mbaya zaidi na muovu zaidi Marekani ndio ulioko madarakani
May 13, 2020 09:11Rais Hassan Rouhani amesema, utawala mbaya zaidi na muovu zaidi Marekani ndio ulioko madarakani na akaongeza kuwa, serikali ya Marekani siku zote ni ya kigaidi lakini kiwango hiki hakijawahi kushuhudiwa.