-
Ukosoaji wa Wademocrat kwa mienendo hasi ya kisiasa ya Rais wa Marekani
May 31, 2017 08:46Mienendo iliyo kinyume na taratibu na misimamo iliyoonyeshwa na Rais Donald Trump wa Marekani wakati wa safari yake ya kiduru barani Ulaya, haijalalamikiwa na viongozi na vyombo vya habari vya nje, bali imekosolewa na kulalamikiwa na Wademokrat pia ndani ya Marekani kwenyewe.
-
Ukosoaji mkali wa Ujerumani kwa mkataba wa silaha wa Marekani na Saudi Arabia
May 30, 2017 23:28Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Ujerumani amekosoa vikali mkataba wa silaha kati ya Marekani na utawala wa Saudi Arabia na kueleza kwamba, Washington inaenda katika mkondo usio sahihi.
-
Israel yafaidika na mkataba wa silaha wa Saudia, Marekani
May 29, 2017 03:16Gazeti moja la Kizayuni, limefichua kuwa, katika mkataba wa mabilioni ya dola wa ununuzi silaha baina ya Marekani na Saudia, mashirika ya Israel yatapata faida kubwa sana.
-
Jaafari: Iraq haitounga mkono muungano dhidi ya Iran
May 28, 2017 23:07Waziri wa Mambo ya Nje wa Iraq amesema nchi yake katu haitounga mkono wala kushirikiana na muungano wowote uliopo au utakaoundwa dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Mashambulizi ya anga ya Marekani yaua raia 117 mashariki mwa Syria
May 26, 2017 09:47Mashambulizi ya anga ya Marekani na waitifaki wake yameuawa raia wasiopungua 117 akthari yao wakiwa wawanake na watoto wadogo katika mkoa wa Dayr al-Zawr, mashariki mwa Syria.
-
Wabunge Marekani wapanga kumzuia Trump kuiuzia Saudia silaha
May 26, 2017 03:04Wabunge kadhaa nchini Marekani wanapanga kuanzisha sheria ya kumzuia Rais Donald Trump kuiuzia Saudia baadhi ya silaha.
-
Ukosoaji mkali wa UN kwa uamuzi wa Marekani wa kupunguza bajeti ya mchango wake kwa umoja huo
May 25, 2017 21:55Msemaji wa Umoja wa Mataifa Stéphane Dujarric, amesema pendekezo la serikali ya Rais Donald Trump wa Marekani la kupunguza bajeti ya mchango wa nchi hiyo kwa umoja huo litaufanya uendeshaji wa shughuli za taasisi hiyo ya kimataifa liwe jambo "lisiloyumkinika".
-
Israel: Hatuhitaji baraka za Marekani kughusubu ardhi zaidi za Palestina
May 25, 2017 09:39Waziri wa Vita wa utawala wa Kizayuni wa Israel amesema Tel Aviv haihitaji baraka wala ruhusu ya Marekani ili kuendeleza ujenzi wa vitongoji vipya vya walowezi wa Kiyahudi katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu.
-
Wakili binafsi wa Trump kuongoza jopo lake la utetezi katika faili la "Trump- Russia"
May 25, 2017 03:18Rais Donald Trump wa Marekani amemwajiri wakili wake wa binafsi Marc Kasowitz kuongoza jopo lake la utetezi dhidi ya tuhuma zinazomkabili za kuwepo mahusiano baina ya timu yake ya kampeni za uchaguzi na maafisa wa serikali ya Russia.
-
Vikosi vya ulinzi vya Iraq katika hatari ya mashambulizi ya Marekani
May 24, 2017 23:03Katika hali ambayo harakati ya wananchi ya Hashdu sh-Sha'abi nchini Iraq katika kukabiliana na ugaidi inaendelea kupongezwa na viongozi, wananchi na hata katika fikra za walio wengi, wanamapambano wa harakati hiyo bado wanaendelea kushambuliwa na ndege za kijeshi za Marekani.